1Mala, Noa, Hogla, Milka na Tirsa walikuwa wabinti za Selofehadi. Naye Selofehadi alikuwa mwana wa Heferi mwana wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase mwana wa Yosefu.
2Basi, hao wabinti wane wakamwendea Musa, wakasimama mbele yake na kuhani Eleazari na viongozi wote wa Waisraeli, kwenye mulango wa hema la mukutano, wakasema:
3Baba yetu alikufia katika jangwa na bila mutoto yeyote mwanaume. Yeye hakukuwa kati ya wafuasi wa Kora waliokusanyika mbele ya Yawe, lakini alikufa kutokana na zambi yake mwenyewe. Hakukuwa na mutoto mwanaume.
4Kwa nini basi jina la baba yetu lifutwe katika ukoo wake kwa sababu hakukuwa na mutoto mwanaume? Utupatie urizi pamoja na wandugu za baba yetu.
5Musa akaleta malalamiko yao mbele ya Yawe.
6Yawe akamwambia Musa:
7Wanachosema wabinti za Selofehadi ni kweli; uwape urizi pamoja na wandugu za baba yao, watwae urizi wake.
18Yawe akamwambia Musa: Umutwae Yoshua mwana wa Nuni, mutu mwenye roho nzuri, kisha uweke mikono juu yake, Kwa njia hii, Eleazari atamwongoza Yoshua na Waisraeli wote wanapotoka na wanapoingia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.