1Kisha mambo hayo
nitashusha Roho wangu juu ya watu wote.
Watoto wenu wanaume na wabinti watatabiri,
wazee wenu wataota ndoto,
na vijana wenu wataona maono.
2Hata juu ya watumishi wanaume na wanawake,
nitashusha Roho wangu wakati huo.
3Nitafanya kitambulisho cha ajabu mbinguni na katika dunia;
kutakuwa damu, moto na minara ya moshi.
4Jua litatiwa giza,
na mwezi utakuwa kama damu,
mbele ya kutimia kwa siku ya Yawe,
siku inayokuwa kubwa na ya kutisha.
5Halafu, watu wote watakaoomba kwa jina la Yawe wataokolewa.
Katika mulima Sayuni na Yerusalema,
kutakuwa watu watakaoponyoka,
kama vile Yawe alivyosema:
wale aliowachagua watabaki wazima.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.