1Lakini kwa ngambo yako, ufundishe maneno yale yanayolingana na mafundisho ya kweli.
2Uwaambie wazee wanaume wakuwe wakadirifu, wenye heshima na utaratibu, wenye kukamilika katika imani, katika upendo na uvumilivu.
3Vilevile uwaambie wanawake wazee wakuwe na mwenendo unaostahili kwa watu watakatifu. Hawapaswi kuwa wasingiziaji, wala wasikuwe watumwa wa pombe, lakini wakuwe wenye kutoa mafundisho mazuri.
4Kwa njia hii wataweza kuwafundisha vijana wanawake kuwapenda waume wao na watoto wao,
5na kuwa wenye utaratibu, wenye maisha safi, wenye kutunza nyumba zao vizuri, wema na wenye kutii waume wao, kusudi Neno la Mungu lisitukaniwe.
6Vilevile uwaonye vijana wanaume wakuwe wenye utaratibu katika mambo yote.
7Na wewe unapaswa kuwa mufano katika matendo mema, ukionyesha ukweli na heshima katika mafundisho yako.
8Ufundishe maneno ya kweli watu wasiyoweza kubishia, hata wale wanaokupinga wapate haya kwa kukosewa na neno baya la kusema juu yetu.
9Sherti watumwa watii wabwana wao katika mambo yote na kuwapendeza, wakiepuka kubishana nao
10na kuiba vitu vyao. Lakini wajionyeshe kila mara kuwa waaminifu kamili, kusudi wapate kuheshimisha mafundisho juu ya Mungu Mwokozi wetu katika mambo yote.
11Kwa maana neema ya Mungu inayoleta wokovu kwa watu wote imeonekana waziwazi.
12Neema hii inatufundisha kwamba tuache uovu na tamaa za dunia, na kuishi katika dunia hii ya sasa katika ukadirifu, katika haki na kushikamana na ibada.
13Na hivi tutaishi tukingojea ule uheri tunaoutumainia, wakati utukufu wa Mungu wetu Mukubwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo utakapotokea.
14Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.
15Haya ndiyo maneno unayopaswa kufundisha, ukiwaonya watu na kuwakaripia kwa mamlaka yote. Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.