1Yotamu alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano alipoanza kutawala, alitawala kwa muda wa miaka kumi na sita kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Yerusa binti ya Sadoki.
2Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe kama vile Uzia baba yake alivyotenda. Hakuingia katika hekalu la Yawe. Watu waliendelea kufanya maovu.
3Yotamu alijenga mulango wa kaskazini wa nyumba ya Yawe na kushugulika sana na ujenzi wa ukuta sehemu ya Ofeli.
4Alijenga miji kwenye inchi ya milima ya Yuda, na kwenye pori, akajenga makimbilio na minara katika milima yenye pori.
5Alipigana vita na mufalme wa Amoni na kuwashinda. Katika mwaka ule Waamoni wakamutolea kodi ya kilo elfu tatu na mia ine za feza, toni elfu moja za ngano na kilo elfu moja za shayiri, waliendelea kufanya hivyo katika mwaka wa pili na wa tatu.
6Mufalme Yotamu aliendelea kuwa mwenye nguvu, kwa sababu aliishi kwa kumutii Yawe, Mungu wake.
7Matendo mengine ya Yotamu, vita yake na maongozi yake, yote yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli na Yuda.
8Yotamu alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano alipoanza kutawala, akatawala kwa muda wa miaka kumi na sita kule Yerusalema.
9Akakufa na kuzikwa katika muji wa Daudi. Na Ahazi mwana wake akatawala pahali pake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.