1Neno la Yawe lilimufikia Yeremia mara ingine, wakati alipokuwa angali amefungwa katika baraza la walinzi, kusema hivi:
2Yawe aliyeiumba dunia, Yawe aliyeifanya na kuiimarisha dunia, yule ambaye jina lake ni Yawe, anasema hivi:
3Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.
4Maana Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda zilizobomolewa kwa sababu ya vita.
5Watu watajaribu kupigana na Wakaldea lakini hiyo itakuwa bure, maana mifereji itajaa maiti za watu ambao nitawaua kwa hasira na kasirani yangu. Kwa vile wamefanya uovu huo wote, mimi nitauacha muji huu.
6Hata hivyo, mimi nitauponyesha muji huu na kuwapa watu wake afya; nitawajalia ustawi mwingi na usalama.
7Nitawastawisha tena Wayuda na watu wa Israeli; nitawaimarisha kama walivyokuwa hapo zamani.
8Nitatakasa zambi zao zote na kuwasamehe uovu wao na uasi walionitendea.
9Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.
10Yawe anasema hivi: Katika muji huu ambao munasema kwamba umekuwa ukiwa bila watu wala nyama, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema ambazo ni tupu, bila watu wala nyama, humo kutasikilika tena sauti za vicheko, sauti za furaha,
11sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi:
Mumushukuru Yawe wa majeshi
kwa sababu Yawe ni muzuri,
kwa maana wema wake unadumu milele.
Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.
12Yawe wa majeshi anasema hivi: Pahali hapa ambapo ni jangwa bila watu wala nyama, na katika miji yake yote, patakuwa shamba ambalo wachungaji watakulisha ndani yake makundi yao ya kondoo.
13Katika miji ya inchi yenye milima, katika miji ya Shefela na katika miji ya jangwa la Negebu, katika inchi ya Benjamina, kandokando ya Yerusalema na katika miji ya Yuda, watu watahesabu tena kondoo wao.
–Ni Yawe anayesema.
14Siku zinakuja ambapo nitatimiza ahadi yangu niliyofanya na Waisraeli na Wayuda.
15Katika siku hizo, katika wakati huo, nitaotesha chipukizi wa haki wa uzao wa Daudi. Chipukizi huyo ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.
16Wakati huo inchi ya Yuda itaokolewa na Yerusalema utakuwa salama. Na muji huo utaitwa “Yawe ni Ukombozi Wetu”.
17Maana Yawe anasema hivi: Hakutakosekana hata kidogo mutu wa uzao wa Daudi atakayetawala Waisraeli.
18Vilevile nao makuhani wa ukoo wa Lawi watakuwa pale siku zote kwa kunitumikia wakinitolea sadaka za kuteketezwa na sadaka za unga na kunitolea sadaka milele.
19Neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:
20Yawe anasema hivi: Kama munaweza kuvunja agano langu nililofanya na usiku na muchana kwa jinsi usiku na muchana visikuwe kwa wakati wake,
21ndivyo itakuwa kwa agano nililofanya na mutumishi wangu Daudi. Nilifanya agano na Daudi kwamba atakuwa na mumoja wa uzao wake wa kutawala pahali pake siku zote; vilevile kutakuwa makuhani wa ukoo wa Lawi watakaonitumikia siku zote.
22Kama vile nyota katika anga na muchanga katika bahari visivyoweza kuhesabiwa, ndivyo nitakavyoongeza hesabu ya wazao wa mutumishi wangu Daudi na hesabu ya makuhani wa ukoo wa Lawi.
23Neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:
24Haujasikia namna watu hawa wanavyosema, kwamba mimi Yawe nimewatupilia mbali watu wa Israeli na watu wa Yuda, jamaa mbili nilizochagua? Wamewazarau watu wangu, hata kuwaona kwamba wao si taifa.
25Yawe anasema hivi: Mimi niliweka agano juu ya muchana na usiku na kuweka maagizo ya mbingu na dunia.
26Basi, ndivyo inavyokuwa vilevile: sitawatupa wazao wa Yakobo na Daudi, mutumishi wangu; nitamuchagua mumoja kati ya wazao wake atawale wazao wa Abrahamu, Isaka na Yakobo. Kwa maana nitawarudishia tena hali yao na kuwahurumia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.