1Zaburi ya Asafu.
Mungu anasimamia baraza lake.
Anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu:
2“Mpaka wakati gani mutaendelea kuhukumu bila haki
na kuwapendelea watu waovu?
3Muimarishe sheria yangu kwa wazaifu na wayatima;
muwatendee wasiojiweza na wamasikini kwa haki.
4Muwaokoe wazaifu na wakosefu,
muwaopoe kutoka makucha ya waovu.
5“Lakini ninyi hamujui wala hamufahamu!
Ninyi munatembea katika giza la upotovu!
Misingi yote ya haki katika dunia imetikiswa!
6Mimi nilisema kwamba ninyi ni miungu,
kwamba ninyi wote ni wana wa Mungu Mukubwa!
7Hata hivyo, mutakufa kama watu wote;
mutaanguka kama mukubwa yeyote.”
8Simama sasa, ee Mungu, uuhukumu ulimwengu;
maana mataifa yote ni mali yako.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.