1Yawe aliniambia hivi: Kwenda ununue mukaba na kuuvaa katika kiuno; lakini usiutie ndani ya maji.
2Basi, nikaenda, nikanunua mukaba kama vile Yawe alivyoniagiza, nami nikauvaa katika kiuno.
3Kisha, neno la Yawe lilinifikia kwa mara ya pili kusema hivi:
4Twaa ule mukaba ulioununua na ambao unaouvaa katika kiuno, uende kwenye muto Furati na kuuficha katika pango chini ya jiwe.
5Basi, nikaenda na kuficha ule mukaba karibu na muto Furati, kama vile Yawe alivyoniamuru.
6Kulipokwisha kupita siku nyingi, Yawe akaniambia: Kwenda kwenye muto Furati, utwae ule mukaba niliokuamuru kuuficha huko.
7Basi, nikaenda kwenye muto Furati, nikachimbua na kuuondoa ule mukaba pahali nilipokuwa nimeuficha. Nilipouondoa, niliona kwamba ulikuwa umeharibika kabisa; nao ulikuwa haufai tena.
8Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
9Yawe anasema hivi: Hivi ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha watu Yuda na kiburi kikubwa cha watu wa Yerusalema.
10Watu hawa waovu wanakataa kusikia maneno yangu. Wanaendelea na kufuata mawazo yao wenyewe. Wanaifuata miungu mingine, wanaitumikia na kuiabudu. Hao watakuwa kama mukaba huu ambao haufai kitu.
11Kama vile mukaba unavyoshikamana na kiuno cha mutu, ndivyo nilivyowashikamanisha nami watu wa Israeli na watu wa Yuda, kusudi wajulikane kwa jina langu, wanisifu na kunitukuza. Lakini wao hawakunisikiliza.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Mutungi wa divai na hasira ya Mungu12Uwaambie watu wa Yuda hivi:
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kila mutungi utajazwa divai.
Utakapowaambia hivyo, wao watakujibu hivi: Unazani sisi hatujui kwamba kila mutungi utajazwa divai?
13Nawe utawajibia hivi:
Yawe anasema hivi: Nitawalewesha wakaaji wote wa inchi hii; wafalme wanaotawala kwa kiti cha kifalme cha Daudi, makuhani, manabii na wakaaji wote wa Yerusalema.
14Nitawagonganisha wao kwa wao hata baba na watoto. –Ni ujumbe wa Yawe.– Sitawahurumia, sitawaachilia wala sitawarehemu, mpaka nitakapowaangamiza.
Yeremia anaonya Waisraeli juu ya kiburi15Enyi Waisraeli, musikilize kwa uangalifu,
musikuwe na kiburi maana Yawe anasema nanyi.
16Mumutukuze Yawe, Mungu wenu,
mbele hajawaletea giza,
mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza.
Ninyi mulitazamia mwangaza,
lakini anaugeuza kuwa usiku
anaufanya kuwa giza nzito.
17Na kama musiponisikiliza,
moyo wangu utalia machozi kwenye uficho,
kwa sababu ya kiburi chenu.
Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi,
maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.
Ujumbe wa Mungu kwa jamaa ya kifalme18Muambie mufalme na malkia mama yake hivi:
Mushuke toka kwenye viti vyenu vya kifalme,
maana taji zenu nzuri zimeanguka toka juu ya vichwa vyenu.
19Miji ya Negebu imezungukwa kwa vita;
hakuna anayeweza kuingia ndani yao.
Watu wa Yuda wamekamatwa mateka,
wote kabisa wamepelekwa katika utumwa.
20Inua macho yako, ee Yerusalema!
Angalia! Waadui zako wanakuja kutoka kaskazini.
Kundi ulilopewa liko wapi?
Kundi lako zuri liko wapi?
21Utasema nini juu ya wale uliowazoeza kuwa warafiki zako,
wale ambao wewe mwenyewe uliwafundisha,
watakapokushinda na kukutawala?
Si utashikwa na uchungu
sawa vile mwanamuke anayezaa?
22Nawe utajiuliza hivi katika moyo wako:
Kwa nini mambo haya yamenipata?
Sawa! Ikiwa kanzu yako imepandishwa,
na kutendewa kwa kinguvu,
hayo ni matokeo ya makosa yako mengi sana.
23Mwetiopia anaweza kubadilisha rangi yake,
au chui madoadoa yake?
Nanyi muliozoea kufanya mabaya,
munaweza namna gani kutenda mema?
24Yawe atawasambaza kama maganda
yanayopeperushwa na upepo unaovuma kutoka katika jangwa.
25Yawe anasema:
Hayo ndiyo yatakayokupata,
ni hivi nilivyoamua kukutendea,
kwa sababu umenisahau mimi
na kutegemea miungu ya uongo.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
26Nitapandisha kanzu yako mpaka kwenye kichwa
hata uchi wako upate kuonekana wazi.
27Nimeyaona machukizo yako:
nimeona uzinzi wako na utongozaji wako,
na uasherati wako usiousikilia haya,
unaoufanya juu ya milima na katika mashamba.
Ole kwako wewe Yerusalema!
Mpaka wakati gani utabaki bila kutakaswa?
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.