1Basi wewe mwana wangu, ukuwe hodari kwa njia ya neema uliyopata katika kuungana kwako na Kristo Yesu.
2Wewe umesikia mafundisho niliyotoa mbele ya washuhuda wengi. Nawe sasa uyafundishe kwa watu waaminifu watakaoweza vilevile kuyatoa kwa watu wengine.
3Ushiriki katika mateso kama vile askari mwema wa Kristo Yesu.
4Askari anapokuwa katika vita, hapaswi kushugulika na mambo ya kawaida ya maisha ya wakaaji kama anataka kumupendeza mukubwa wa kundi lake.
5Vilevile mutu yeyote anayeshindana katika michezo hawezi kupata zawadi ya ushindi kama asipotii kanuni za michezo.
6Tena mulimaji anayetumika kazi ngumu ndiye anayepaswa kupata sehemu ya kwanza ya mavuno.
7Ufikiri juu ya maneno hayo ninayosema, kwa maana Bwana atakupa uwezo kwa kuyaelewa yote.
8Umukumbuke Yesu Kristo aliyekuwa wa ukoo wa mufalme Daudi, na aliyefufuka sawa vile inavyotangazwa na Habari Njema hii ninayohubiri.
9Mimi ninateswa na kufungwa sawa mutenda maovu kwa sababu ninahubiri Habari Njema hii. Lakini Neno la Mungu halifungwi.
10Ni kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya watu ambao Mungu alijichagulia kuwa wake, kusudi wao vilevile wapate kuokoka na kupata utukufu wa milele unaopatikana kwa njia ya Kristo Yesu.
11Maneno haya ni ya kuaminiwa:
Kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye vilevile.
12Kama tunaendelea kuvumilia, tutatawala pamoja naye vilevile.
Kama tunamukana, naye atatukana vilevile.
13Kama tunakosa kuwa waaminifu, yeye anabaki mwaminifu.
Kwa maana hawezi kujikana yeye mwenyewe.
Mutumishi mwema14Uwakumbushe watu maneno hayo yote na kuwaonya wazi mbele ya Mungu waache kubishana juu ya maneno. Mabishano hayana faida kwa maana yanawapoteza wale wanaoyasikia.
15Ufanye juhudi kusudi upate kuhesabiwa mbele ya Mungu kama mutu anayemupendeza, ukiwa kama mutumishi asiyesikia haya juu ya kazi yake, lakini anayetangaza kwa haki ujumbe wa kweli wa Mungu.
16Uepuke masemi yasiyokuwa na maana na ya kidunia, kwa maana wale wanaoyafuata wanazidi kupotoka katika ibada ya uongo.
17Maneno yao yanaambukiza kama vile kidonda chenye kuoza kinavyoharibu mwili wote. Kati yao kuna Himeneo na Fileto.
18Hao wamepotoka mbali na ukweli, wamepotosha imani ya watu wengi wakisema kwamba ufufuko tunaongojea umekwisha kufanyika.
19Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule “Bwana anajua wale wanaokuwa wake,” na haya mengine: “Kila mutu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.”
20Ndani ya nyumba kubwa, hamuna vyombo vya zahabu na feza tu, lakini muko vilevile vyombo vya miti na vya udongo. Vimoja ni vya matumizi ya kipekee na vingine ni vya matumizi ya kawaida.
21Basi kama mutu atajitakasa kwa kujitenga na maovu hayo yote atakuwa chombo cha matumizi ya kipekee, kitakatifu cha mwenye nyumba na chenye mafaa kwake na kuwa tayari kwa kila kazi njema.
22Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi.
23Ukatae mabishano ya kipumbafu na yasiyokuwa na maana; unajua wewe mwenyewe kwamba yanaleta magomvi.
24Basi, mutumishi wa Bwana hapaswi kugombana. Anapaswa kuwa mupole kwa watu wote, anayejua kufundisha na muvumilivu.
25Anapaswa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye; kwa maana labda Mungu anaweza kuwajalia hata wapate kugeuka toka zambi na kutambua ukweli.
26Kwa njia hiyo wanaweza tena kupata ufahamu na kuponyoka katika mitego ya Shetani, aliyewanasa na kuwafanya watimize mapenzi yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.