1Rehoboamu alipofika Yerusalema, alikusanya waaskari wafundi wa vita elfu mia moja na makumi nane wa makabila ya Yuda na Benjamina, apate kupigana na utawala wa Israeli, kusudi aurudishe utawala kwake yeye mwenyewe Rehoboamu.
2Lakini neno la Yawe lilimufikia Semaya, yule mutu wa Mungu, kusema hivi:
3“Umwambie Rehoboamu mwana wa Solomono, mufalme wa Yuda na Waisraeli wote katika Yuda na Benjamina kwamba
4Bwana anasema hivi: ‘Musiende wala musipigane na wandugu zenu. Murudie kila mutu kwake, maana yale yaliyotokea ni kwa kufuata mupango wangu.’ ” Basi wakatii ujumbe wa Yawe, wakarudia kila mutu kwake, wala hawakwenda kupigana na Yeroboamu.
Rehoboamu anaimarisha miji5Rehoboamu alikaa Yerusalema na akajenga kuta kwa kuimarisha miji hii iliyokuwa katika inchi ya Yuda:
6Betelehemu, Etamu, Tekoa,
7Beti-Suri, Soko, Adulamu,
8Gati, Maresa, Zifu,
9Adoraimu, Lakisi, Azeka,
10Zora, Ayaloni na Hebroni. Miji hiyo yenye kuzungukwa kuta iko Yuda na Benjamina.
11Aliziimarisha kuta zile na mule ndani akaweka majemadari na magala ya vyakula, mafuta na divai.
12Ndani ya kila muji, aliweka ngao na mikuki, na kuifanya miji hiyo kuwa imara sana. Yuda na Benjamina zikakuwa chini ya mamlaka yake.
Makuhani na Walawi wanahamia katika inchi ya Yuda13Makuhani na Walawi wote waliokuwa wanaishi kote katika inchi ya Israeli, wote wakavuka mupaka wao na kumwendea.
14Walawi wakaacha mashamba yao ya malisho ya nyama, na maeneo yao mengine kwa sababu Yeroboamu na wana wake waliwakataza kumutumikia Yawe kama vile makuhani wa Yawe.
15Yeroboamu akajichagulia makuhani wake mwenyewe wa kutumika kwenye nafasi za ibada za miungu na wa kuabudu mizimu na sanamu za wana-ngombe alizojitengenezea. Ang. 1 Fal 12.31
16Watu wote ambao walikuwa wamekusudia kwa moyo kumwabudu Yawe, Mungu wa Israeli, kutoka katika makabila yote ya Israeli, waliandamana na Walawi mpaka Yerusalema kusudi wapate kumutolea sadaka Yawe, Mungu wa babu zao.
17Hivyo, wakaimarisha ufalme wa Yuda, na kwa muda wa miaka mitatu, wakauunga mukono utawala wa Rehoboamu mwana wa Solomono, ukakuwa imara na wakaishi katika hali ileile waliyoishi wakati walipokuwa chini ya utawala wa mufalme Daudi na mufalme Solomono.
Jamaa ya Rehoboamu18Rehoboamu alioa muke, jina lake Mahalati binti ya Yeremoti mwana wa Daudi. Mama yake aliitwa Abihaili binti ya Eliabu, mwana wa Yese.
19Naye akamuzalia wana watatu: Yeusi, Semaria na Zahamu.
20Kisha, akamwoa Maka binti ya Abusaloma, naye akamuzalia Abiya, Atai, Siza na Selomiti.
21Rehoboamu alioa wake kumi na wanane na wahabara makumi sita, akazaa wana makumi mbili na wane na wabinti makumi sita. Kati ya wake zake wote na wahabara wake, alimupenda zaidi Maka binti ya Abusaloma.
22Hivyo akamuchagua Abiya, mwana wa Maka, kuwa mukubwa kati ya wandugu zake, maana alikusudia kumufanya kuwa mufalme.
23Rehoboamu alifanya jambo la hekima, akawatawanya wamoja kati ya wana wake katika inchi yote ya Yuda na Benjamina akiwaweka katika miji yote yenye kuzungukwa na kuta. Wakiwa mule, akawapa vyakula vingi na vilevile akawaoea wake wengi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.