Matayo 15 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Desturi za babu(Mk 7.1-13)

1Wafarisayo na walimu wa Sheria wakamufikia Yesu kutoka Yerusalema. Basi wakamwuliza:

2“Kwa sababu gani wanafunzi wako wanavunja desturi za babu zetu kwa kula chakula pasipo kunawa mikono?”

3Yesu akawajibu: “Na ninyi, kwa sababu gani munavunja amri ya Mungu kwa kufuata desturi zenu?

4Kwa maana Mungu alisema: ‘Uwaheshimu baba yako na mama yako.’ Naye alisema vilevile: ‘Anayelaani baba yake au mama yake anapaswa kuuawa.’

5Lakini ninyi munasema kwamba mutu akiwa na kitu ambacho angeweza kuwasaidia baba yake au mama yake, lakini akimwambia kwamba amekitoa sadaka kwa Mungu,

6basi, hapaswi tena kumusaidia baba yake. Hivi munazarau Neno la Mungu kwa kufuata desturi zenu.

7Ninyi wanafiki! Isaya alitabiri vema juu yenu, wakati aliposema maneno haya:

8‘Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao.

Lakini mioyo yao ni mbali nami.

9Ibada wanayonifanyia ni ya bure,

sababu mafundisho yao yanalingana na kanuni za watu tu.’ ”

Vitu vinavyomuchafua nutu(Mk 7.14-23)

10Kisha Yesu akaita kundi la watu na kuwaambia: “Musikilize na kuelewa maneno nitakayowaambia.

11Kitu kinachoingia ndani ya kinywa cha mutu hakiwezi kumuchafua. Lakini ni kile kinachotoka ndani ya kinywa chake ndicho kinachomuchafua.”

12Halafu wanafunzi wakamufikia na kumwuliza: “Unajua kwamba Wafarisayo walikwazwa kwa kusikia maneno hayo uliyosema?”

13Yesu akajibu: “Wao ni kama mumea usiopandwa na Baba yangu wa mbinguni, utakaopaswa kuongolewa.

14Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”

15Halafu Petro akamwambia: “Utuelezee maana ya mufano huu.”

16Yesu akamujibu: “Hata ninyi vilevile hamuwezi kuelewa?

17Hamwelewi kwamba kila kitu kinachoingia ndani ya kinywa, kinapita ndani ya tumbo na kisha kinatoka na kwenda katika choo?

18Lakini vyote vinavyotoka ndani ya kinywa ni vyenye kutoka kwanza ndani ya moyo wake, navyo vinamuchafua mutu.

19Kwa maana ndani ya moyo munatoka mawazo mabaya yanayoleta uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo na matukano.

20Mambo haya ndiyo yanayomuchafua mutu! Lakini kula pasipo kunawa mikono hakuwezi kumuchafua mutu.”

Imani ya mwanamuke Mukanana(Mk 7.24-30)

21Yesu akaondoka pale na kwenda pande za karibu na muji wa Tiro na wa Sidona.

22Mwanamuke mumoja Mukanana aliyeishi katika pande zile akamufikia, akilalamika, akisema: “Ee Bwana, mwana wa Daudi, unihurumie! Binti yangu anateswa sana na pepo.”

23Lakini Yesu hakumujibu hata neno moja. Halafu wanafunzi wake wakamufikia na kumusihi: “Umwambie aende kwa maana anatuuzi na makelele.”

24Naye Yesu akajibu: “Nimetumwa tu kwa taifa la Waisraeli, wanaokuwa kama kondoo wanaopotea.”

25Lakini mwanamuke yule akapiga magoti mbele yake na kumwambia: “Ee Bwana, unisaidie!”

26Yesu akamujibu: “Si vizuri kukamata chakula cha watoto na kukitupia imbwa.”

27Yule mwanamuke akasema: “Ndiyo, Bwana, unasema ukweli, lakini hata imbwa wanazoea kula makombo yanayoanguka chini ya meza ya wabwana wao.”

28Halafu Yesu akamujibu: “Wewe mwanamuke, imani yako ni kubwa! Ifanyike kwako sawa ulivyoomba.”

Na binti yake akapona tangia saa ile ile.

Yesu anawaponyesha watu wengi

29Yesu akaondoka kule, akapita pembeni ya ziwa la Galilaya. Kisha akapanda kwenye kilima, naye akaikaa pale.

30Halafu makundi mengi ya watu wakamufikia, wakimuletea vilema, vipofu, viwete na wabubu. Wakawaweka mbele ya Yesu, naye akawaponyesha.

31Yale makundi ya watu wakashangaa sana wakati walipowaona wabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanatembea, na vipofu wanaona. Nao wakamusifu Mungu wa Waisraeli.

Yesu anakulisha watu elfu ine(Mk 8.1-10)

32Yesu akawaita wanafunzi wake, na kuwaambia: “Ninawasikilia watu hawa huruma, kwa sababu wamekaa nami sasa kwa muda wa siku tatu, nao hawana chakula tena. Nami sitaki kuagana nao pasipo kula, kusudi wasiregee katika njia.”

33Nao wanafunzi wake wakamujibu: “Hapa katika pori, tutaweza kupata wapi chakula cha kushibisha kundi kubwa kama hili?”

34Yesu akawauliza: “Muko na mikate ngapi?”

Nao wakajibu: “Tuko na mikate saba na samaki ndogo chache.”

35Basi Yesu akawaamuru watu waikae chini.

36Kisha akatwaa ile mikate saba na zile samaki, akamushukuru Mungu, akaimega na kuwapa wanafunzi wake wavigawanye kwa watu.

37Wote wakakula na wakashiba. Kisha wanafunzi wakaokota vipande vilivyobaki, wakajaza vitunga saba.

38Watu waliokula walikuwa wanaume elfu ine, pasipo kuhesabu wanawake na watoto.

39Kisha kuaga yale makundi ya watu, Yesu akaingia ndani ya chombo, na kwenda pande za Magadani.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help