1“Makuhani Walawi, ni kusema kabila lote la Lawi, wasikuwe na sehemu wala urizi katika Israeli. Wao watakula sehemu ya sadaka za Yawe.
2Wala wasikuwe na urizi kati ya wandugu zao; Yawe ndiye urizi wao kama vile alivyoahidi.
3“Na hii itakuwa haki ya makuhani kutoka kwa watu wanaotolea sadaka ikuwe ni ngombe au kondoo: watamupa kuhani muguu wa mbele, mashavu na matumbotumbo.
4Mutawapa sehemu ya kwanza ya mazao yenu ya ngano, divai, mafuta yenu na sufu ya kwanza ya kondoo wenu.
5Katika makabila yenu yote, Yawe amechagua kabila la Walawi limutumikie kama vile makuhani milele.
6“Ikiwa Mulawi yeyote atapenda mwenyewe anaweza kutoka katika muji wowote wa Israeli kwenda pale pahali Yawe alipochagua,
7na hapo anaweza kutumika kwa jina la Yawe, Mungu wake, kama wale Walawi wengine wanaotumika mbele ya Yawe.
8Watapata mafungu yao sawa ya kula, ingawa wako na mapato kutokana na kuuzisha mali za jamaa zao.
Onyo juu ya desturi ngeni9“Mutakapofika katika ile inchi Yawe, Mungu wenu, anayowapa, musifuate zile tabia za kuchukiza za mataifa ya huko.
10Kusikuwe mutu yeyote kati yenu anayemupitisha kwenye moto mutoto wake mwanaume au mwanamuke kuwa tambiko, wala mutu anayepiga ramuli, wala mwaguzi, wala mwenye kufanya uganga,
11wala muchawi, wala mulozi, wala mwenye kutaka shauri kwa mizimu na pepo au kutoka kwa wafu.
12Maana yeyote anayetenda mambo haya ni chukizo kwa Yawe; na kwa ajili ya mambo haya ya kuchukiza Yawe, Mungu wenu, anafukuza watu wa namna hiyo mbele yenu.
13Mukuwe wakamilifu mbele ya Yawe, Mungu wenu.
14Kwa maana mataifa haya ambayo mutairizi inchi yao wanafuata maongozi ya waaguzi na wapiga ramuli; lakini Yawe, Mungu wenu hawaruhusu ninyi kufanya hivyo.
Ahadi ya kupewa nabii15“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.
16Hicho ndicho mulichomwomba Yawe, Mungu wenu, kule Horebu, siku ile mulipokusanyika na kusema: ‘Tusisikie tena sauti ya Yawe, Mungu wetu, wala tusiuone tena moto huu mukubwa, kusudi tusikufe!’
17Naye Yawe akaniambia: ‘Wamesema ukweli.
18Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.
19Yeyote ambaye hatasikia maneno nabii huyo atakayosema kwa jina langu, mimi mwenyewe nitamwazibu.
20Lakini nabii yeyote atakayesema kwa jina la miungu mingine, au atakayejaribu kusema neno kwa jina langu wakati mimi sikumwambia aseme, huyo nabii atakufa.’
21“Lakini ninyi munaweza kusema: ‘Tutaweza namna gani kutambua neno ambalo Yawe hakulisema?’
22Kama nabii akisema kitu aseme ni kwa jina la Yawe, na kitu hicho hakifanyiki au hakiko kweli, jambo hilo Yawe hakulisema; nabii amelisema kwa kiburi, nanyi musitishwe na jambo hilo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.