1 Mambo ya Siku 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Uzao wa Adamu(Mwa 5.1-32; 10.1-32; 11.10-26)

1-4Hawa ndio babu wa kwanza waliofuatana kwa kila kizazi:

Adamu

Seti

Enosi

Kenani

Mahalaleli

Yaredi

Hanoki

Metusela

Lameki

Noa

Wana wa Noa walikuwa: Semu, Hamu na Yafeti.

5Wana wa Yafeti walikuwa: Gomeri, Magogi, Madayi, Yavani, Tubali, Meseki na Tirasi.

6Wana wa Gomeri walikuwa: Askenazi, Rifati na Togarma.

7Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarsisi, Kitimu na Roda.

8-10Wana wa Hamu walikuwa baba za watu walioishi katika inchi ya Etiopia, Misri, Puti na Kanana.

Wana wa Etiopia walikuwa: Seba, Havila, Sabuta, Rama na Sabuteka. Etiopia alizaa vilevile Nimurodi, aliyekuwa mutu shujaa wa kwanza katika dunia.

Wana wa Rama walikuwa: Seba na Dedani.

11Wazao wa Misri ni: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanafutuhi,

12Wapatirusi Wakafutori na Wakasiluhi (hao ndio asili ya Wafilistini).

13Wana wa Kanana walikuwa: Sidoni, muzaliwa wake wa kwanza, na Heti.

14Kanana vilevile ndiye babu ya Wayebusi, Waamori, Wagirgasi,

15Wahivi, Waarki, Wasini,

16Waarwadi, Wasemari na Wahamati.

17Wana wa Semu walikuwa: Elamu, Asuri, Arpakisadi, Ludi, Aramu, Usi, Huli, Geteri na Meseki.

18Arpakisadi alikuwa baba ya Sela.

Sela alikuwa baba ya Eberi.

19Eberi alikuwa na wana wawili: mumoja wao aliitwa Pelegi, ni kusema “Matengano”, kwa maana wakati wake watu walikuwa wametawanyika katika dunia, na ndugu yake aliitwa Yokitani.

20Wana wa Yokitani walikuwa: Almodadi, Selefu, Hazarmaweti, Yera,

21Hadoramu, Uzali, Dikla,

22Ebali, Abimaeli, Seba,

23Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote ni wana wa Yokitani.

24-27Semu alikuwa baba ya Arpakisadi,

Arpakisadi baba ya Sela,

Sela baba ya Eberi,

Eberi baba ya Pelegi,

Pelegi baba ya Reu,

Reu baba ya Serugi,

Serugi baba ya Nahori,

Nahori baba ya Tera,

Tera baba ya Abramu, ambaye ndiye Abrahamu.

28Abrahamu alikuwa na wana wawili: Isaka na Isimaeli.

Isimaeli alikuwa baba ya:

29Nebayoti, ndiye muzaliwa wake wa kwanza, Kedari, Abudeli, Mibusami,

30Misima, Duma, Masa, Hadadi, Tema,

31Yeturi, Nafisi na Kedema. Hao ndio wana wa Isimaeli.

32Abrahamu alikuwa na habara aliyeitwa Ketura. Ketura alimuzalia Abrahamu: Simurani, Yokisanu, Medani, Midiani, Isibaki na Sua.

Wana wa Yokisanu walikuwa: Seba na Dedani.

33Wana wa Midiani walikuwa: Efa, Eferi, Hanoki, Abida na Eldaa. Wote hawa walikuwa wana wa Ketura.

34Isaka, mwana wa Abrahamu, alikuwa na wana wawili: Esau na Israeli.

35Wana wa Esau walikuwa: Elifasi, Rueli, Yeusi, Yalamu na Kora.

36Wana wa Elifasi walikuwa: Temani, Omari, Zefi, Gatamu, Kenasi, Timuna na Amaleki.

37Wana wa Rueli walikuwa: Nahati, Zera, Sama na Miza.

38Wana wa Seiri walikuwa: Lotani, Zobali, Sibeoni, Ana, Disoni, Ezeri na Disani.

39Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Lotani alikuwa na dada yake aliyeitwa Timuna.

40Wana wa Sobali walikuwa: Aliani, Manahati, Ebali, Sefi na Onamu.

Wana wa Sibeoni walikuwa: Aya na Ana.

41Mwana wa Ana alikuwa: Disoni.

Wana wa Disoni walikuwa: Hamurani, Esibani, Itirani na Kerani.

42Wana wa Ezeri walikuwa: Bilihani, Zawani na Yakani.

Wana wa Disoni walikuwa: Usi na Arani.

Wafalme wa Edomu(Mwa 36.31-43)

43-50Hawa ndio wafalme waliotawala katika inchi ya Edomu mbele mufalme yeyote hajatawala Waisraeli:

Bela mwana wa Beori, akiwa na makao yake makubwa katika muji wa Dinihaba.

Yobabu mwana wa Zera kutoka muji wa Boza.

Husamu wa inchi ya Watani.

Hadadi mwana wa Bedadi, makao yake makubwa yakiwa katika muji wa Awiti. Huyu ndiye aliyepiga na kushinda Wamidiani katika inchi ya Moabu.

Samula kutoka muji wa Masireka.

Saulo kutoka muji wa Rehoboti unaokuwa, karibu na muto Furati.

Bali-Hanani mwana wa Akibori.

Hadadi kutoka muji wa Pai. Jina la muke wake ni Mehetabeli, binti ya Matiredi na mujukuu wa Mesahabu.

51-54Nyuma ya kifo cha Hadadi, inchi ya Edomu ilitawaliwa na wakubwa hawa:

Timuna, Aiya, Yeteti,

Oholibama, Ela, Pinoni,

Kenasi, Temani, Mibusari,

Magdieli na Irama.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help