1 Wakorinto 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Salamu

1Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Sositeni. Ni mimi niliyeitwa na Mungu kwa mapenzi yake kuwa mutume wa Kristo Yesu.

2Tunawaandikia ninyi kanisa la Mungu linalokuwa Korinto, ninyi ambao mumetakaswa kwa njia ya kuungana kwenu na Yesu Kristo na mumeitwa na Mungu kuwa watu wake. Vilevile barua hii ni kwa wote wanaoabudu jina la Bwana Yesu Kristo fasi zote, anayekuwa Bwana wao na Bwana wetu vilevile.

3Tunawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.

Baraka tunazopewa kwa njia ya Kristo

4Ninamushukuru Mungu wangu siku zote kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema Mungu aliyowapa ninyi kwa njia ya Yesu Kristo.

5Kwa maana katika kuungana kwenu na Kristo, mumejaliwa katika vitu vyote, zaidi sana katika mambo yanayoelekea masemi na ufahamu.

6Ile inatokana na vile ujumbe juu ya Kristo umehakikishwa kwa nguvu kati yenu,

7hata hamukosewi zawadi yoyote ya Mungu, mukiwa mukingojea wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakapoonekana.

8Ni yeye atakayewasimamisha ninyi imara mpaka mwisho kusudi musishitakiwe juu ya kosa lolote Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

9Mungu ni mwaminifu katika ahadi zake, yeye aliyewaita ninyi muishi katika ushirika pamoja na Mwana wake Yesu Kristo, Bwana wetu.

Matengano katika kanisa

10Wandugu zangu, ninawasihi ninyi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mukuwe na masikilizano kusudi matengano yasikuwe katikati yenu. Muishi katika umoja kabisa mukiwa na nia moja na wazo moja.

11Kwa maana, wandugu zangu, nimepata habari zenu kwa njia ya jamaa ya Kloe kwamba kuko ugomvi katikati yenu.

12Ninataka kusema: kila mumoja kati yenu anasema maneno yake mbalimbali. Mumoja anasema: “Mimi ni wa Paulo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Petro,” na mwingine anasema: “Mimi ni wa Kristo.”

13Munafikiri kwamba Kristo amegawanyika? Paulo ndiye aliyetundikwa juu ya musalaba kwa ajili yenu? Au mumebatizwa kwa jina la Paulo?

14Ninamushukuru Mungu kuwa sikubatiza hata mumoja wenu isipokuwa Krispo na Gayo.

15Hivi hakuna anayeweza kusema kwamba amebatizwa kwa jina langu.

16Ni kweli, nilibatiza vilevile jamaa ya Stefano, zaidi ya wale sikumbuki kama nilibatiza mutu mwingine.

17Kristo hakunituma kwa kubatiza, lakini amenituma kwa kutangaza Habari Njema. Amenituma kuitangaza bila kutumia hekima ya usemi, kusudi uwezo unaotokana na kufa kwa Kristo juu ya musalaba usihesabiwe kuwa bure.

Yesu Kristo ni uwezo na hekima ya Mungu

18Hivi, mahubiri ya kufa kwa Kristo juu ya musalaba yanahesabiwa kuwa upumbafu kwa wale wanaopotea. Lakini kwa sisi tunaookolewa ni uwezo wa Mungu.

19Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema:

“Nitaharibu hekima ya wenye hekima,

Nitapoteza akili ya wenye akili.”

20Basi, tuseme nini juu ya wenye hekima, walimu wa Sheria, nao wafundi wa usemi siku hizi? Mungu ameonyesha wazi kwamba hekima ya dunia hii ni upumbafu!

21Mungu alikusudia kuwaokoa wale wanaomwamini kwa njia ya mahubiri tunayotangaza yanayoonekana kuwa mambo ya upumbafu. Amefanya vile kwa sababu, kwa njia ya hekima yao ya kimutu, watu hawakumutambua Mungu na hekima yake ya kimungu.

22Wayuda wanaomba kuonyeshwa vitambulisho nao Wagriki wanatafuta hekima.

23Lakini sisi tunamuhubiri Kristo aliyetundikwa juu ya musalaba, na mahubiri hayo yanahesabiwa kama kikwazo kwa Wayuda na upumbafu kwa watu wa mataifa mengine.

24Lakini kwa wale walioitwa na Mungu, ikiwa Wayuda au wasiokuwa Wayuda, Kristo ni kitambulisho cha uwezo na hekima ya Mungu.

25Kwa maana mambo wanayomuhesabilia Mungu kuwa ya upumbafu, yanapita hekima ya watu; nayo mambo yale wanayomuhesabilia kuwa ya uzaifu yanapita nguvu za watu.

26Basi wandugu zangu, mukumbuke vile mulivyoitwa na Mungu, kwamba si wengi kati yenu wenye hekima kufuatana na mafikiri ya watu; si wengi kati yenu wanaokuwa wenye nguvu, wala wenye vyeo.

27Lakini Mungu anachagua vitu ambavyo watu wanahesabu kuwa vya upumbafu kusudi apatishe wenye hekima haya, naye amechagua vitu wanavyohesabu kuwa vya uzaifu kusudi apatishe wenye nguvu haya.

28Mungu amechagua vitu ambavyo watu wanahesabu kuwa vya hali ya chini na vyenye kuzarauliwa, visivyokuwa na maana mbele ya macho ya watu, kusudi aharibu vile wanavyohesabu kuwa vya lazima.

29Alifanya vile kusudi hata mutu mumoja asijivune mbele yake.

30Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.

31Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Anayetaka kujivuna, ajivune kwa ajili ya Bwana.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help