Zaburi 20 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kuomba ushindi

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.

2Yawe akujibu unapokuwa katika taabu;

jina la Mungu wa Yakobo likulinde.

3Akupelekee musaada kutoka katika hekalu lake;

akukinge tokea kwenye mulima Sayuni.

4Akumbuke sadaka zako zote;

akubali sadaka zako za kuteketezwa.

5Akujalie unayotamani ndani ya moyo wako,

afanikishe mipango yako yote.

6Tutashangilia kwa ajili ya ushindi wako;

tutainua bendera kwa kutukuza jina la Mungu wetu.

Yawe akutimizie mapenzi yako yote!

7Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua,

atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni;

kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.

8Wamoja wanajivunia magari ya vita, wengine farasi wao.

Lakini sisi tunajivunia Yawe, Mungu wetu.

9Hao wanajikwaa na kuanguka;

lakini sisi tunasimama na kuimarika.

10Ee Yawe, umujalie mufalme ushindi,

utujibu wakati tunapokuomba.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help