1Sasa musikilize, enyi wakubwa wa wazao wa Yakobo,
musikilize, enyi watawala wa wazao wa Israeli!
Ninyi ndio munaopaswa kujua namna ya kufuata sheria ya Mungu.
2Lakini ninyi munachukia mazuri na kupenda mabaya.
Munawachuna ngozi watu wangu,
na kunyofoa nyama juu ya mifupa yao.
3Munajikulisha kwa nyama ya watu wangu,
munawachuna ngozi yao,
munaivunjavunja mifupa yao,
na kuwakatakata kama nyama ya kupika,
kama nyama ya kutia ndani ya chungu.
4Wakati unakuja ambapo mutamulilia Yawe,
lakini yeye hatawajibu.
Atauficha uso wake wakati huo,
kwa sababu mumetenda mambo maovu.
5Yawe anasema hivi
juu ya manabii wanaowapotosha watu wake,
manabii ambao wanatabiri amani wakipewa kitu,
lakini wanawatishia watu kwa vita wasipopewa kitu:
6Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono,
kutakuwa giza kwenu bila ufunuo.
Jua litatua juu yenu,
na muchana utakuwa giza kwenu.
7Waonaji watafezeheka,
waaguzi watapata haya;
wote watafunga midomo yao,
maana hawatapata jibu lolote kutoka kwa Mungu.
8Lakini kwa upande wangu,
nimejazwa nguvu na roho ya Yawe;
nimejaliwa kufuata sheria ya Mungu na kuwa na uwezo
niwatangazie wazao wa Yakobo kosa lao,
niwaambie Waisraeli zambi yao.
9Musikie jambo hili, enyi waongozi wa wazao wa Yakobo,
musikilize, enyi watawala wa Waisraeli:
Ninyi munachukia sheria ya Mungu
na kupotosha mambo ya usawa.
10Ninyi munajenga Sayuni kwa damu,
Yerusalema kwa uovu.
11Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro,
makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo,
manabii wanatabiri kwa kupata feza.
Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe,
wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi?
Hatutapatwa na hasara yoyote!
12Basi! Kwa sababu yenu,
Sayuni utalimwa kama shamba,
Yerusalema lundo la makokoto,
nao mulima wa hekalu utakuwa pori.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.