1Kila mara nikitaka kurudishia watu wangu hali yao ya mbele,
ninapotaka kuwaponyesha Waisraeli,
uovu wa watu wa Efuraimu unafunuliwa,
matendo mabaya ya Samaria yanajitokeza.
Wao wanaongozwa na udanganyifu,
mwizi anabomoa nyumba;
inje katika barabara wanyanganyi wanashambulia.
2Hawafikiri hata kidogo kwamba mimi
ninayakumbuka maovu yao yote.
Sasa maovu yao yamewabana.
Yote waliyotenda yako mbele yangu.
Uovu katika nyumba ya kifalme3Wanamufurahisha mufalme, lakini ni waovu;
wanawafurahisha wakubwa, lakini ni wanafiki.
4Wote ni wazinzi;
wao ni kama furu iliyowashwa moto
ambayo mutengenezaji wa mikate haichochei tangia wakati anapoponda unga
mpaka mikate itakapovimba.
5Kwenye sikukuu ya mufalme,
waliwalewesha sana wakubwa wake;
naye mufalme akashirikiana na watu wa ovyoovyo.
6Kama vile furu inavyowaka ndivyo mioyo yao inavyowaka kwa udanganyifu;
usiku kucha hasira yao inafukiza moshi,
inapofika asubui, inawaka kama ndimi za moto.
7Wote wamewaka hasira kama furu,
na wanawaangamiza watawala wao.
Wafalme wao wote wameanguka,
wala hakuna anayeniomba musaada.
Israeli anategemea mataifa mengine,8Efuraimu amechanganika na watu wa mataifa.
Anaonekana kama mukate ambao haukugeuzwa.
9Wageni wamenyonya nguvu zake,
wala yeye mwenyewe hajui;
imvi zimejaa juu ya kichwa chake,
lakini yeye mwenyewe hana habari.
10Kiburi cha Waisraeli kinawashuhudia wao wenyewe,
hawanirudilii mimi Yawe, Mungu wao;
wala hawanitafuti kwa ajili ya matukio hayo yote.
11Efuraimu ni kama njiwa mujinga asiyekuwa na akili;
mara yuko Misri, mara Asuria kwa kuomba musaada.
12Watakapokwenda nitatandaza wavu wangu niwanase,
nitawaangusha chini kama ndege toka katika anga;
nitamwaazibu kufuatana na jinsi walivyotangaza kwa kusanyiko lao.
13Ole kwao kwa sababu wameniacha!
Maangamizi yawapate, maana wameniasi.
Nilitaka kuwakomboa,
lakini wanasema uongo juu yangu.
14Wananililia, lakini si kwa moyo.
Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao,
kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai;
lakini wanaendelea kuniasi.
15Mimi ndimi niliyeiimarisha mikono yao,
lakini wanafikiri maovu juu yangu.
16Wanaigeukia miungu ya bure,
wako kama upinde ulioregea.
Waongozi wao watakufa kwa upanga,
kwa sababu ya maneno yao ya kiburi.
Kwa hiyo, watazarauliwa katika inchi ya Misri.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.