2 Wafalme 6 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Shoka linapatikana

1Siku moja, wanafunzi wa manabii walimulalamikia Elisha wakisema: “Pahali hapa tunapokaa ni padogo sana kwetu!

2Uturuhusu tuende Yordani tukate kila mutu muti mumoja kusudi tujijengee pahali pa kututoshelea.”

Elisha akawajibu: “Mwende.”

3Mumoja wao akamwomba akisema: “Tafazali ninakusihi uende pamoja na watumishi wako.”

Naye akajibu: “Nitakwenda.”

4Hivyo akaenda pamoja nao, na walipofika kwenye muto Yordani wakaanza kukata miti.

5Mumoja wao alipokuwa anakata miti, shoka lake likachomoka na kuanguka ndani ya maji. Akalia, akisema: “Sasa bwana wangu nitafanya nini? Shoka hili tulikuwa tumeliazima!”

6Elisha akauliza: “Liliangukia wapi?”

Mutu huyo akamwonyesha. Elisha akakata kijiti na kukitupa ndani ya maji na palepale shoka likaelea juu ya maji.

7Elisha akamwamuru alikamate naye akanyoosha mukono, akalikamata.

Waaskari wa Waaramu wanashindwa

8Wakati mumoja kulikuwa vita kati ya Aramu na Israeli. Basi, mufalme wa Aramu akafanya shauri na wakubwa wa waaskari wake juu ya pahali watakapopiga kambi.

9Lakini Elisha akamupelekea mufalme wa Israeli habari afanye angalisho na pahali pale, kwa sababu Waaramu walikuwa tayari kupashambulia.

10Basi, mufalme wa Israeli akapeleka waaskari wake karibu na pahali alipoambiwa. Elisha aliendelea kumwonya mufalme naye mufalme alijiweka katika hali ya angalisho. Jambo hilo lilifanyika mara nyingi.

11Mufalme wa Aramu akafazaishwa sana na hali hiyo. Akawaita wakubwa wa waaskari wake, akawauliza: “Muniambie ni nani kati yenu anayekuwa upande wa mufalme wa Israeli?”

12Mumoja wao akajibu: “Hakuna anayekuwa upande wake, ee mufalme. Anayefanya vile ni Elisha, nabii anayekuwa kule Israeli. Yeye anamwambia mufalme wa Israeli mambo yote unayosema hata ukiwa katika chumba chako cha kulala.”

13Mufalme akawaambia: “Mwende mupeleleze mujue pahali anapokuwa nami nitawatuma watu wamukamate.”

Basi, wakamwambia kwamba Elisha alikuwa kule Dotani.

14Kwa hiyo mufalme akatuma kule kundi kubwa la waaskari pamoja na farasi na magari ya vita. Kundi hilo likafika kule wakati wa usiku na kuuzunguka muji.

15Mutumishi wa Elisha alipoamuka mapema kesho yake na kutoka inje, akaona waaskari pamoja na farasi na magari ya vita wameuzunguka muji. Akarudi ndani akasema: “Ole wetu, ee, Bwana wangu! Sasa tutafanya nini?”

16Elisha akamujibu: “Usiogope kwa sababu wanaokuwa pamoja nasi ni wengi kuliko wanaokuwa pamoja nao.”

17Kisha Elisha akaomba: “Ee Yawe, umufumbue macho kusudi apate kuona!”

Basi, Yawe akamufumbua macho yule kijana, akaona farasi na magari ya moto yakiwa kila pahali katika mulima wote, kumuzunguka Elisha.

18Waaramu waliposhambulia, Elisha alimwomba Yawe akisema: “Ninakuomba ufanye watu hawa wakuwe vipofu!” Yawe akasikiliza ombi lake na kuwafanya vipofu.

19Halafu Elisha akawaendea na kuwaambia: “Mumepotea njia. Huu siyo muji ambao munautafuta. Munifuate nami nitawapeleka kwa yule munayemutafuta.” Naye akawaongoza mpaka Samaria.

20Mara tu walipoingia katika muji, Elisha akaomba, akisema: “Ee Yawe, uwafumbue macho kusudi waone.” Yawe akasikia ombi lake, akawafumbua macho. Nao wakajikuta wako katikati ya muji wa Samaria.

21Mufalme wa Israeli alipowaona Waaramu, alimwuliza Elisha: “Niwaue?”

22Elisha akajibu: “Hapana, usiwaue. Maana hawa unaotaka kuwaua uliwateka kwa upanga wako na mushale wako? Uwape chakula na maji, wakule na kunywa kisha uwaache warudie kwa bwana wao.”

23Mufalme wa Israeli akawafanyia karamu kubwa. Walipomaliza kula na kunywa, akawarudisha kwa bwana wao. Toka wakati ule, Waaramu hawakuishambulia tena inchi ya Israeli.

Muji wa Samaria unazungukwa kwa vita

24Nyuma ya hayo, mufalme Beni-Hadadi wa Aramu akakusanya waaskari wake wote akatoka na kuuzunguka muji wa Samaria.

25Matokeo yake ilikuwa njaa kali katika muji wa Samaria. Kichwa cha punda kilinunuliwa kwa vikoroti makumi tatu vya feza, na grama mia moja za mavi ya njiwa zilinunuliwa kwa vikoroti vitano vya feza.

26Siku moja mufalme wa Israeli alipokuwa anatembea juu ya ukuta wa muji, alisikia mwanamuke mumoja akimwita: “Unisaidie, ee bwana wangu mufalme!”

27Mufalme akamwambia: “Yawe asipokusaidia, mimi nitaweza kukupa musaada kutoka wapi? Kutoka katika kiwanja cha kupepetea ngano au kutoka katika kikamulio?

28Shida yako ni nini?”

Akamujibu: “Juzi mwanamuke huyu alinishauria tumukule mwana wangu na kesho yake tutamukula wake.

29Tukamupika mwana wangu, tukamukula. Kesho yake nikamwambia tumukule mwana wake, lakini alikuwa amemuficha!”

30Mara mufalme aliposikia maneno ya mwanamuke yule alipasua nguo zake kwa huzuni, na watu waliokuwa karibu na ukuta waliona kwamba alikuwa amevaa nguo ya gunia ndani yake.

31Naye akasema: “Mungu aniue Elisha mwana wa Safati asipokatwa kichwa leo!”

32Halafu akatuma mujumbe kwenda kumuleta Elisha.

Wakati uleule, Elisha alikuwa ndani ya nyumba pamoja na wazee waliomutembelea. Mbele ya kufika kwa mujumbe wa mufalme, Elisha akawaambia wazee: “Yule mwuaji amemutuma mutu kuja kunikata kichwa! Atakapofika hapa, mufunge mulango, wala musimuruhusu aingie. Vilevile bwana wake anamufuata nyuma.”

33Mbele hata hajamaliza kusema, mufalme akafika, akasema: “Mabaya haya yametoka kwa Yawe! Nitangojea nini tena kutoka kwake?”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help