Wimbo wa Solomono 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Mimi ni kama ua la Saroni,

ni yungiyungi ya mabonde.

Masemi ya mume

2Kama yungiyungi kati ya michongoma,

ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa kati ya wabinti.

Masemi ya muke

3Kama muti wa matunda kati ya miti ya pori,

ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa kati ya vijana.

Ninafurahia kuikaa chini ya kivuli chake,

na tunda lake tamu sana kwangu.

4Alinipeleka mpaka katika chumba cha karamu,

akapandisha bendera ya mapenzi juu yangu.

5Munishibishe na zabibu kavu,

munifurahishe kwa matunda,

maana ninaugua kwa mapenzi!

6Mukono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu,

mukono wake wa kuume unanikumbatia.

7Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema,

kama vile paa au swala wanavyokuwa katika pori,

musichochee wala kuamusha mapenzi,

mpaka pale wakati wake utakapofika.

Shairi la piliMasemi ya muke

8Hiyo ni sauti ya mupenzi wangu,

yeye anakuja mbio,

anaruka milima,

vilima anavipita haraka!

9Mupenzi wangu ni kama paa,

ni kama swala muchanga.

Anasimama karibu na ukuta wetu,

anachungulia kwenye dirisha,

anaangalia kwenye wavu.

10Mupenzi wangu ananiambia, akisema:

Masemi ya mume

Simama basi, ewe mupenzi wangu, unayependeza,

kuja tuende zetu.

11Wakati wa baridi umepita,

nazo mvua zimekwisha kukoma;

12maua yamechanua kila pahali.

Wakati wa kuimba umefika;

sauti za njiwa zinasikilika katika mashamba yetu.

13Miti ya tini imeanza kuzaa

na mizabibu imechanua.

Inatoa harufu nzuri.

Kuja, basi, ewe mupenzi wangu unayenipendeza,

kuja tuende.

14Ee njiwa yangu, uliyejificha

katika matundu kwenye mulima,

uniache kuona uso wako

na kusikia sauti yako,

maana sauti yako ni nzuri

na uso wako unapendeza.

15Mutukamatie mbweha,

wale mbweha wadogowadogo,

wanaoharibu mizabibu yetu inayochanua.

Masemi ya muke

16Mupenzi wangu ni wangu, nami ni wake.

Yeye anakulisha kondoo wake penye yungiyungi.

17Mpaka pale jua linapochomoza

na vivuli kutoweka,

rudi kama paa, mupenzi wangu,

kama swala mudogo juu ya milima ya Beteri.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help