1Mimi ni kama ua la Saroni,
ni yungiyungi ya mabonde.
Masemi ya mume2Kama yungiyungi kati ya michongoma,
ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa kati ya wabinti.
Masemi ya muke3Kama muti wa matunda kati ya miti ya pori,
ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa kati ya vijana.
Ninafurahia kuikaa chini ya kivuli chake,
na tunda lake tamu sana kwangu.
4Alinipeleka mpaka katika chumba cha karamu,
akapandisha bendera ya mapenzi juu yangu.
5Munishibishe na zabibu kavu,
munifurahishe kwa matunda,
maana ninaugua kwa mapenzi!
6Mukono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu,
mukono wake wa kuume unanikumbatia.
7Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema,
kama vile paa au swala wanavyokuwa katika pori,
musichochee wala kuamusha mapenzi,
mpaka pale wakati wake utakapofika.
Shairi la piliMasemi ya muke8Hiyo ni sauti ya mupenzi wangu,
yeye anakuja mbio,
anaruka milima,
vilima anavipita haraka!
9Mupenzi wangu ni kama paa,
ni kama swala muchanga.
Anasimama karibu na ukuta wetu,
anachungulia kwenye dirisha,
anaangalia kwenye wavu.
10Mupenzi wangu ananiambia, akisema:
Masemi ya mumeSimama basi, ewe mupenzi wangu, unayependeza,
kuja tuende zetu.
11Wakati wa baridi umepita,
nazo mvua zimekwisha kukoma;
12maua yamechanua kila pahali.
Wakati wa kuimba umefika;
sauti za njiwa zinasikilika katika mashamba yetu.
13Miti ya tini imeanza kuzaa
na mizabibu imechanua.
Inatoa harufu nzuri.
Kuja, basi, ewe mupenzi wangu unayenipendeza,
kuja tuende.
14Ee njiwa yangu, uliyejificha
katika matundu kwenye mulima,
uniache kuona uso wako
na kusikia sauti yako,
maana sauti yako ni nzuri
na uso wako unapendeza.
15Mutukamatie mbweha,
wale mbweha wadogowadogo,
wanaoharibu mizabibu yetu inayochanua.
Masemi ya muke16Mupenzi wangu ni wangu, nami ni wake.
Yeye anakulisha kondoo wake penye yungiyungi.
17Mpaka pale jua linapochomoza
na vivuli kutoweka,
rudi kama paa, mupenzi wangu,
kama swala mudogo juu ya milima ya Beteri.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.