Zaburi 52 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Hukumu ya Mungu

1-2Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Daudi yanayoelekea wakati Doegi wa Edomu alipomwendea Saulo na kumujulisha kwamba Daudi amemwendea Ahimeleki.

3Mbona, ewe jitu,

unajivunia mabaya unayotendea waaminifu.

4Kila wakati unawaza maangamizi.

Ulimi wako ni kama wembe mukali.

Unafikiria tu kutenda mabaya.

5Wewe unapenda ubaya kuliko uzuri,

unapenda uongo kuliko ukweli.

6Ewe mudanganyifu mukubwa,

unapenda mambo ya kuangamiza wengine.

7Kwa hiyo Mungu atakuangamiza milele,

atakunyanyua na kukuondoa katika nyumba yako;

atakuongoa katika inchi ya wenye kuishi.

8Watu wa haki wataona, wataogopa,

na kisha watakuchekelea na kusema:

9“Muangalie yaliyomupata mutu huyu!

Yeye hakutaka Mungu akuwe kimbilio lake,

lakini alitegemea wingi wa mali yake,

na kutafuta humo usalama wake!”

10Lakini mimi ni kama muzeituni mubichi,

unaostawi katika nyumba ya Mungu.

Ninategemea wema wake milele na milele.

11Ee Mungu, nitakushukuru siku zote,

kwa ajili ya mambo uliyofanya.

Nitatangaza kwamba wewe ni muzuri,

mbele ya watu wako waaminifu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help