Kutoka 13 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kutakaswa kwa wazaliwa wa kwanza

1Yawe alimwambia Musa:

2“Unitakasie wazaliwa wote wa kwanza, maana wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli ni wangu, ikuwe wanaume au wanyama.” Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu

3Musa akawaambia watu: “Mukumbuke siku hii muliyotoka inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Yawe alipowatoa humo kwa mukono wake wenye nguvu. Katika siku hii, musikule mukate uliotiwa chachu.

4Siku hii, mwezi wa kwanza wa Abibu, mutaondoka katika inchi ya Misri.

5Na wakati Yawe atakapowafikisha katika inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Wahivi, na Wayebusi, inchi ambayo aliwaapia babu zenu kwamba atawapa ninyi, inchi inayotiririka maziwa na asali, munapaswa kushika sikukuu hii kila mwaka katika mwezi huu wa kwanza.

6Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu, na katika siku ya saba mutafanya sikukuu kwa heshima ya Yawe.

7Kwa muda ule wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu. Kusikuwe mikate iliyotiwa chachu, wala chachu yoyote kati yenu na katika inchi yenu yote.

8Siku hiyo mutawaambia watoto wenu kwamba munafanya hivyo kwa sababu ya jambo Yawe alilowafanyia mulipoondoka katika inchi ya Misri.

9Na mambo haya yatakuwa ukumbusho, kama vile kitambulisho katika mikono yenu au katika paji la nyuso zenu; kusudi kiwakumbushe siku zote sheria ya Yawe. Maana, Yawe amewatoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.

10Kwa hiyo, mutashika sikukuu hii kwa wakati uliopangwa, kila mwaka.”

Maelezo juu ya wazaliwa wa kwanza

11Musa akaendelea kuwaambia watu: “Vilevile, wakati Yawe atakapowafikisha katika inchi ya Wakanana na kuwapa inchi ile kama vile alivyowaapia ninyi na babu zenu,

12munapaswa kumuwekea Yawe kila muzaliwa wenu wa kwanza mwanaume. Kila muzaliwa wa kwanza dume wa mifugo yenu atakuwa wa Yawe. Waisraeli wakaondoka katika inchi ya Misri wakiwa wamejitayarisha kwa vita.

19Musa alipeleka mifupa ya Yosefu kama vile Yosefu alivyoagiza mbele ya kufa kwake. Alikuwa amewaapisha Waisraeli akisema: “Mungu atakapowafikia kuwatoa katika inchi hii, munapaswa kupeleka mifupa yangu kutoka hapa pamoja nanyi.”

20Basi, Waisraeli wakaondoka Sukoti, wakapiga kambi kule Etamu, kwenye ukingo wa jangwa.

21Muchana, Yawe aliwatangulia katika munara wa wingu kwa kuwaonyesha njia. Na usiku aliwatangulia katika munara wa moto kuwaangazia, kusudi waweze kusafiri muchana na usiku.

22Munara wa wingu wakati wa muchana na munara wa moto wakati wa usiku haikukosekana kuwatangulia Waisraeli.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help