1Solomono, mwana wa mufalme Daudi, alijiimarisha katika utawala wake, naye Yawe, Mungu wake akamubariki na kumufanya akuwe mukubwa sana.
2Mufalme Solomono aliita majemadari wote wa vikundi vya maelfu na vya mamia, waamuzi, viongozi wote wa ukoo za Waisraeli.
3Kisha akaandamana nao mpaka pahali pa ibada kule Gibeoni. Walikwenda kule kwa sababu pale ndipo pahali palipokuwa hema la mukutano la Mungu ambalo Musa mutumishi wa Yawe, alilotengeneza katika jangwa.
4(Lakini, sanduku la Mungu lilikuwa Yerusalema katika hema ambalo mufalme Daudi alilipigia alipolileta kutoka Kiriati-Yearimu). Ang. 2 Sam 6.1-17; 1 Sik 13.5-14; 15.25–16.1
5Tena, mazabahu ya shaba iliyotengenezwa na Bezaleli, mwana wa Uri na mujukuu wa Huri, ilikuwa kule Gibeoni mbele ya hema takatifu la Yawe. Hapo mufalme Solomono na watu wote wakamwomba Yawe. Ang. Kut 38.1-7
6Solomono akapanda mbele ya mazabahu ya shaba iliyokuwa kwenye hema la mukutano. Pale mbele ya Yawe, akatoa sadaka elfu moja za kuteketezwa juu ya mazabahu yale.
7Usiku ule, Mungu akamutokea Solomono, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka, nami nitakupa.”
8Solomono akamwambia Mungu: “Ulimutendea baba yangu Daudi mema mengi, na umenijalia kuwa mufalme kwa pahali pake.
9Sasa, ee Mungu, Yawe, utimize ahadi uliyomupa Daudi baba yangu. Umeniweka kuwa mufalme juu ya watu hawa wanaokuwa wengi kama mavumbi. Ang. Mwa 13.16; 28.14
10Kwa hiyo, ninakuomba unipe hekima na maarifa kusudi niweze kuwatawala watu wako vizuri. Kama sivyo, nitaweza namna gani kuwatawala hawa watu wako wanaokuwa wengi hivi?”
11Mungu akamujibu Solomono: “Kwa sababu jambo hili uliloomba liko ndani ya moyo wako, na wala haukuomba mali, wala utajiri, wala heshima wala haukuomba wanaokuchukia waangamizwe, wala maisha marefu, lakini umeomba hekima na maarifa kusudi uwatawale vizuri watu wangu ambao nimekupa ukuwe mufalme wao,
12ninakupa hekima na maarifa. Vilevile, nitakupa utajiri, mali na heshima zaidi ya mufalme mwingine yeyote aliyekuwa mbele yako na mufalme mwingine yeyote atakayetawala nyuma yako.”
Utajiri na uwezo wa mufalme Solomono(1 Fal 10.26-29)13Basi, Solomono akaondoka pahali pale pa kuabudia, kule Gibeoni, kulipokuwa hema la mukutano, akarudi Yerusalema. Akatawala inchi ya Israeli.
14Solomono alikusanya magari ya vita na waaskari wapanda-farasi; alikuwa na magari ya vita elfu moja na mia ine, na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili. Aliwaweka katika miji yenye vituo vya magari ya vita na kwake katika Yerusalema. Ang. 1 Fal 4.26
15Mufalme Solomono aliongeza feza na zahabu zikakuwa nyingi kama mawe katika Yerusalema, na mbao za mierezi zikapatikana kwa wingi kama mikuyu ya Sefela.
16Farasi wa Solomono walitoka Misri na Kilikia; wachuuzi wake waliwanunua toka kule. Ang. Kumb 17.16
17Walinunua gari moja la vita kutoka Misri kwa bei ya vikoroti mia sita za feza, na farasi mumoja kwa vikoroti mia moja na makumi tano za feza. Kisha waliwauzishia wafalme wa Wahiti na wa Wasuria farasi hao na magari.
Matayarisho ya kujenga hekalu(1 Fal 5.1-18)18Mufalme Solomono akakusudia kujenga nyumba ambamo Yawe ataabudiwa, na vilevile kujijengea yeye mwenyewe nyumba ya kifalme.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.