Kutoka UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002

UTANGULIZIJina la kitabu hiki “KUTOKA” ni tafsiri ya jina la Kigriki “eksodos” ambalo linaelekea tukio kubwa kabisa katika historia ya watu wa Israeli: kuondolewa kwao katika utumwa kule Misri, kuvuka bahari Nyekundu, na safari yao katika jangwa mpaka kwenye mulima Sinai. Kitabu hiki kinagawanyika katika sehemu tano:Sura 1–18: Kukombolewa toka utumwa wa Misri na safari mpaka kwenye mulima Sinai. Katika sehemu hii tunapata habari juu ya kugandamizwa kwa Waisraeli kule Misri, halafu kwa mara ya kwanza Musa anatajwa, naye ni wa ukoo wa Lawi. Mungu alijijulisha kwa Musa kama “Mimi ndimi ninayekuwa” musemo ambao labda ndio unaokuwa kiini cha jina “Yawe”. Mungu alimupatia Musa kazi ya kumwambia mufalme wa Misri kuwaachilia Waisraeli waondoke. Mufalme wa Misri akakataa na hapo tunaambiwa juu ya “mapigo” kumi na kuondoka kwa Waisraeli. Kisha tunapata habari juu ya kuanzishwa kwa sikukuu ya Pasaka, juu ya kuvuka bahari Nyekundu na kufika katika jangwa la Sinai.Sura 19–24: Kukutana kwa Mungu na watu wa Israeli na kuwekwa kwa uhusiano kati yake nao. Pale Waisraeli wanapewa mwongozo wa maisha – amri kumi na maagizo mbalimbali juu ya maisha ya kawaida na ibada. Kisha tunajulishwa jinsi agano kati ya Mungu na watu wale lilivyofanywa.Sura 25–31: Katika sehemu hii tunaelezwa jinsi Musa alivyoagizwa na Mungu kutengeneza hema takatifu (hema la mukutano) na Sanduku la Agano.Sura 32–34: Sehemu hii inaelekea uasi wa Waisraeli walipojitengenezea sanamu ya mwana-ngombe na kuiabudu wakati Musa alipokuwa amekwenda kuzungumuza na Mungu juu ya mulima Sinai (Musa aliwaambia waziwazi kwamba Mungu hawezi kufananishwa na kiumbe chochote).Sura 36–40: Hapa tunapata habari zaidi juu ya hema takatifu na kutakaswa kwake. Katika hema hilo Mungu alikutana mara kwa mara na Musa.
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help