1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi. Wimbo.
2Utuonee huruma, ee Mungu, utubariki,
utuelekezee uso wako kwa wema,
3dunia yote ipate kutambua njia yako,
mataifa yote yajue nguvu yako ya kuokoa.
4Watu wakusifu, ee Mungu,
watu wote wakusifu!
5Mataifa yote yafurahi na kuimba kwa furaha;
maana unawahukumu watu kwa usawa,
na kuyaongoza mataifa katika dunia.
6Watu wakusifu, ee Mungu,
watu wote wakusifu!
7Inchi imetoa mazao yake;
Mungu, Mungu wetu, ametubariki.
8Mungu aendelee kutubariki.
Watu wote katika dunia wamwabudu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.