1Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.
2Mupumbafu hapendezwi na ufahamu; kitu cha maana kwake ni maoni yake tu.
3Mwovu anapokuja, mazarau yanakuja vilevile; pamoja na haya, matusi yanakuja.
4Maneno ya kinywa cha mutu ni kilindi cha maji; chemichemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.
5Si vizuri kumupendelea mutu mwovu, na kumunyima sheria mutu wa haki.
6Maneno ya mupumbafu yanaleta ugomvi; kila neno analosema linasababisha azabu.
7Kinywa cha mupumbafu kinamwangamiza mwenyewe; mudomo wake ni mutego wa kumunasa yeye mwenyewe.
8Maneno ya muchongeaji ni kama chakula kitamu ambacho kinashuka mpaka ndani kabisa ya tumbo.
9Mutu muvivu katika kazi yake ni ndugu ya muharibifu.
10Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama.
11Tajiri anazani kwamba mali ni makimbilio yake; anafikiri hayo ni ukuta murefu unaomulinda.
12Majivuno ya ndani ya moyo yanaleta maangamizi, lakini unyenyekevu unaleta heshima.
13Kujibu mbele ya kusikiliza ni upumbafu na jambo la haya.
14Roho ya mutu inaweza kuvumilia ugonjwa, lakini ukiwa umevunjika moyo, utavumilia namna gani?
15Mutu mwenye akili anajipatia maarifa; sikio la mwenye hekima linatafuta maarifa.
16Zawadi inamufungulia mutu milango; inaweza kumufikisha mutu mbele ya mukubwa.
17Anayejitetea wa kwanza anaonekana kuwa na haki, mpaka pale mupinzani wake atakapoanza kumupinga.
18Kura inakomesha ubishi; inaamua kati ya wakubwa wanaopingana.
19Ndugu aliyetendewa kosa ni mugumu kuliko muji wenye ukuta; magomvi yanakaza kama vile vifungio vya mulango wa ukuta.
20Maneno ya mutu yanaweza kumushibisha; anatosheka kwa matokeo ya maneno yake.
21Ulimi una nguvu ya kuleta uzima na kuua; wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.
22Anayemupata muke amepata kizuri; ni zawadi kutoka kwa Yawe.
23Masikini anaomba kwa unyenyekevu, lakini tajiri anajibu kwa ukali.
24Warafiki wengi wanaweza kumwangusha mutu, lakini kuna rafiki mwaminifu kuliko ndugu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.