1Wimbo wa safari za kidini.
Kila mutu katika Israeli aseme:
“Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu”.
2Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu,
lakini hawakunishinda.
3Walinikata vidonda katika mugongo,
kama wanavyolima matuta katika shamba.
4Lakini Yawe ni mwenye haki;
ametutosha katika utumwa wa hao waovu.
5Wafezeheke na kurudishwa nyuma,
wote wale wanaouchukia Sayuni.
6Wakuwe kama nyasi juu ya paa la nyumba,
ambazo zinanyauka mbele ya kukomaa,
7anayezikata hajazi kitanga cha mukono,
wala anayezikusanya haenezi fungu.
8Naye anayepita karibu asiwaambie:
“Yawe awabariki!
Tunawabariki kwa jina la Yawe!”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.