Kumbukumbu la Sheria 16 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Pasaka(Kut 12.1-20)

1“Mushike mwezi wa Abibu na kufanya Pasaka kwa heshima ya Yawe, Mungu wenu. Maana katika mwezi huo wa Abibu, Yawe, Mungu wenu aliwatoa Misri wakati wa usiku.

2Mutatoa sadaka ya Pasaka kutoka mifugo yenu ya kondoo au ngombe kwa heshima ya Yawe pahali ambapo Yawe atachagua kwa ajili ya jina lake.

3Musikule sadaka hiyo na mikate iliyotiwa chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso – kwa sababu mulitoka Misri kwa haraka; kwa hiyo, muda wote mutakaoishi mutakumbuka ile siku mulipotoka Misri.

4Kwa muda wa siku saba mutu yeyote katika inchi yenu asiweke chachu ndani ya nyumba yake, na nyama ya yule nyama aliyechinjwa magaribi ya siku ya kwanza isibaki mpaka asubui.

5Musitolee sadaka ya Pasaka katika muji wowote ambao Yawe, Mungu wenu, atawapa;

6lakini mutaitolea pale pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake. Mutatolea sadaka ya Pasaka magaribi, jua linapotua, wakati uleule mulipotoka Misri.

7Hiyo nyama mutaipika na kuikula pahali pale Yawe, Mungu wenu atakapochagua. Asubui yake mutageuka na kurudi katika mahema zenu.

8Katika siku sita mutakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya saba kutakuwa mukutano mukubwa wa kumwabudu Yawe, na hamutafanya kazi yoyote katika siku hiyo.

Sikukuu ya mavunno(Kut 34.22)

9“Mutahesabu majuma saba; mutaanza kuyahesabu tangu munapoanza kuvuna ngano.

10Halafu mutafanya sikukuu ya majuma kwa heshima ya Yawe, Mungu wenu, kwa kutoa sadaka ya mapenzi kadiri Yawe, Mungu wenu, anavyowabariki.

11Mutafurahia mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi pamoja nanyi. Mufanye haya katika pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake.

12Mukumbuke kwamba mulikuwa watumwa kule Misri na mukuwe waangalifu kufuata masharti haya.

Sikukuu ya vibanda(Law 23.33-43; Hes 29.12-39)

13“Kisha kupepeta ngano yenu yote na kukamua zabibu zenu, mutafanya sikukuu ya vibanda kwa muda wa siku saba.

14Mutafanya karamu hiyo, ninyi na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.

15Kwa siku saba mutamufanyia Yawe, Mungu wenu, karamu pahali ambapo Yawe atachagua; kwa sababu Yawe, Mungu wenu atawabariki kwa mazao yenu yote na katika shuguli zenu zote nanyi hakika mutafurahi.

16“Wanaume wote wa taifa lenu watakuja mbele ya Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka, pahali ambapo Yawe, Mungu wenu atachagua: wakati wa sikukuu ya Pasaka, sikukuu ya kuvuna na wakati wa sikukuu ya vibanda. Wasitokee mbele ya Yawe mikono mitupu.

17Wote watatoa kadiri wanavyoweza kulingana na baraka Yawe, Mungu wenu, alizowajalia.

Maagizo juu ya haki

18“Mutachagua waamuzi na wakubwa kutoka makabila yenu katika miji yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapa nao watatoa hukumu za haki kwa watu.

19Musipotoshe haki, musikuwe na upendeleo, wala musikubali kupokea kituliro, kwa kuwa kituliro kinapofusha macho ya watu wenye hekima na kupotosha maneno ya mutu mwenye haki.

20Mutafuata yanayokuwa ya haki tu, kusudi mupate kuishi na kurizi inchi munayopewa na Yawe, Mungu wenu.

21“Musipande muti wowote ukuwe nguzo ya mungu wa uongo karibu na mazabahu mutakayomujengea Yawe, Mungu wenu.

22Wala musisimamishe nguzo ambayo Yawe Mungu wenu anaichukia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help