Isaya 22 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Ujumbe wa Mungu juu ya Yerusalema

1Ujumbe wa Mungu juu ya Bonde la Maono.

Kuna nini, ee Yerusalema?

Mbona watu wote mumepanda juu ya nyumba?

2Kwa nini munapiga kelele za shangwe,

na muji wote umechangamuka na kujaa vigelegele?

Watu wenu waliokufa hawakuuawa katika vita,

wala hawakuuawa katika mapigano.

3Wakubwa wenu wote walikimbia,

wakakamatwa hata mbele ya kufyatua mushale mumoja.

Watu wako wote waliopatikana walitekwa,

ingawa walikuwa wamekimbilia mbali.

4Ndiyo maana ninawaambia ninyi:

musijali chochote juu yangu,

muniache nilie machozi ya uchungu.

Musijisumbue kunifariji

kwa ajili ya kuangamizwa kwa watu wangu.

5Maana leo Yawe wa majeshi

ametuletea fujo,

kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono.

Kuta za muji zimebomolewa.

Kilio cha wakaaji wake kinasikilika mpaka kwenye milima.

6Majeshi ya Elamu, pinde na mishale katika mikono,

walikuja wamepanda farasi na magari ya vita;

nalo jeshi la Kiri lilitayarisha ngao zake.

7Mabonde yako mazuri, ewe Yerusalema,

yalijaa magari ya vita na farasi;

wapanda-farasi walijipanga tayari kwenye milango yako.

8Ulinzi wote wa Yuda uliporomoka.

Siku hiyo mulikwenda kutafuta silaha zilizokuwa zimelindwa katika Nyumba ya Pori,

9mukaona kwamba nyufa za kuta za muji wa Daudi ni nyingi, mukajaza maji ndani ya birika la chini.

10Mulizikagua nyumba za Yerusalema, mukazibomoa kwa kupata mawe ya kukaza kuta za muji.

11Katikati ya kuta hizo mulijijengea birika la kulinda maji yanapotiririka kutoka birika la zamani. Lakini hamukumutafuta Mungu aliyepanga mambo haya yote; hamukumujali yeye aliyepanga hayo yote tangu zamani.

12Siku hiyo, Yawe wa majeshi

alitaka mulie na kuomboleza,

munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.

13Lakini ninyi mukafurahi na kusherehekea.

Mulichinja ngombe na kondoo,

mukakula nyama na kunywa divai.

Ninyi mulisema:

Acha tukule na kunywa

maana kesho tutakufa.

14Yawe wa majeshi alinifunulia haya akisema:

Hakika uovu huu hautasahauliwa

mbele ya kufa kwenu.

Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.

Ujumbe wa Mungu juu ya Sebuna

15Bwana wetu Yawe wa majeshi aliniambia niende kwa Sebuna, musimamizi wa jamaa ya kifalme, nimwambie hivi:

16Una haki gani kuwa huku? Una ndugu yeyote hapa, hata ukajichongea kaburi ndani ya jiwe juu ya mulima?

17Wewe bwana, Yawe atakutupilia mbali kwa nguvu. Atakubana kabisa

18na kukuzungushazungusha, kisha atakutupa kama mupira mpaka katika inchi pana. Huko utakufia karibu na magari yako ya vita unayojivunia, wewe unayezaraulisha nyumba ya bwana wako.

19Yawe atakuongoa toka katika madaraka yako na kukuporomosha kutoka pahali unapokuwa.

20Siku hiyo, nitamuleta mutumishi wangu Eliakimu mwana wa Hilkia.

21Nitamuvalisha nguo yako ya heshima, na mukaba wako na kumupa madaraka yako. Yeye atakuwa baba kwa watu wa Yerusalema na kwa ukoo wa Yuda.

22Nitaweka juu ya bega lake ufunguo wa ukoo wa Daudi. Akifungua, hakuna atakayeweza kufunga na akifunga, hakuna atakayeweza kufungua.

23Nitamwimarisha Eliakimu kama musumari uliopigiliwa pahali pagumu, naye atapata heshima tukufu katika ukoo wa wazee wake.

24Watu wote na jamaa yake, wadogo kwa wakubwa watajitegemeza kwake kama chungu na vikombe vilivyotundikwa kwenye musumari.

25Lakini siku moja, –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi– ule musumari uliopigiliwa pahali pagumu utaregea kwa uzito. Utakatwa na kuanguka. Yawe amesema.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help