Wakolosayi 4 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Ninyi wabwana muwatendee watumishi wenu kwa usawa na kwa haki, mukijua kwamba ninyi vilevile muko na Bwana wenu katika mbingu.

Maonyo

2Mudumu katika kuomba. Munapoomba mukeshe na kumutolea Mungu shukrani.

3Mutuombee sisi vilevile kusudi Mungu atufungulie njia ya kuhubiri neno lake tupate kutangaza ujumbe wa siri juu ya Kristo. Ni kwa ajili ya ujumbe ule mimi niko sasa katika kifungo.

4Basi muniombee kusudi nipate kuupasha waziwazi sawa ninavyopaswa kufanya.

5Mukuwe na mwenendo wa hekima mbele ya watu wanaokuwa wa inje ya kanisa, mukitumia vema kila wakati munaoupata.

6Masemi yenu yanapaswa kuwa mazuri siku zote na yenye kufaa, munapaswa kujua kujibia kila mutu vizuri.

Salamu za mwisho

7Ndugu yetu mupendwa Tikiko mutumishi mwaminifu, na mwenzangu tunayetumika naye kazi ya Bwana atawapasha ninyi habari zangu zote.

8Ni kwa shabaha hiyo ninamutuma kwenu apate kuwajulisha habari zetu na kuwafariji.

9Ninamutuma pamoja na ndugu mupendwa na mwaminifu, Onesimo, anayekuwa mwanainchi wa kule kwenu. Wao ndio watawaelezea maneno yote yaliyotokea hapa.

10Mufungwa mwenzangu Aristarko anawasalimia. Naye Marko, binamu wa Barnaba anawasalimia vilevile. (Mumekwisha kupata maagizo juu ya Marko; akifika kwenu mumupokee vizuri).

11Naye Yesu anayeitwa Yusto, anawasalimia ninyi vilevile. Kati ya Wayuda walioamini ni hao watatu tu ndio wanaotumika pamoja nami kwa ajili ya kazi inayoelekea Ufalme wa Mungu, nao wamenifariji sana.

12Mwanainchi mwenzenu Epafra anawasalimia vilevile. Yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, hachoki kwa kuwaombea ninyi, kusudi musimame imara mukikomaa kiroho na kuwa tayari kwa kutimiza kabisa mapenzi ya Mungu.

13Ninaweza kushuhudia juu yake kwamba anajisumbua sana kwa ajili yenu na kwa ajili ya wandugu wa Laodikia na wa Hierapoli.

14Luka, muganga wetu mupendwa na Dema wanawasalimia.

15Muwasalimie wandugu wa Laodikia, pamoja na Nimfa na kanisa linalokusanyika ndani ya nyumba yake.

16Barua hii itakapokwisha kusomwa kwenu mufanye namna yote ipate kusomwa vilevile katika kanisa la Laodikia. Na ninyi kwa ngambo yenu, musome vilevile barua niliyotuma kwa kanisa lile.

17Mumwambie Arkipo aangalie vizuri atimize kazi ile aliyopewa na Bwana.

18Mimi Paulo ninawatumia salamu zangu, nikiziandika kwa mukono wangu mwenyewe. Musisahau kwamba mimi ningali katika kifungo.

Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help