1-3Hawa ndio wana wa mufalme Daudi waliozaliwa wakati alipokuwa kule Hebroni:
Amunoni, muzaliwa wake wa kwanza. Mama yake aliitwa Ahinoamu, wa muji wa Yezereheli;
wa pili: Danieli ambaye mama yake aliitwa Abigaili wa muji wa Karmeli;
wa tatu: Abusaloma, ambaye mama yake aliitwa Maka, binti ya Talmai mufalme wa Gesuri;
wa ine: Adonia, ambaye mama yake aliitwa Hagiti;
wa tano: Sefatia, ambaye mama yake aliitwa Abitali;
wa sita: Itiramu, ambaye mama yake aliitwa Egla.
4Wote sita, walizaliwa Hebroni ambako Daudi alitawala kwa muda wa miaka saba na nusu.
Kule Yerusalema, alitawala kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu.Ang. 2 Sam 5.4,5; 1 Fal 2.11; 1 Sik 29.27
5Hawa ndio wana wa mufalme Daudi waliozaliwa alipokuwa Yerusalema:
Muke wake Bati-Seba, binti ya Amieli, akamuzalia wana wane: Simea, Sobabu, Natani na Solomono.2 Sam 11.3
6Na zaidi ya hao alikuwa na wana wengine tisa: Ibuhari, Elisua, Elifeleti,
7Noga, Nefegi, Yafia,
8Elisama, Eliada na Elifeleti.
9Hao wote walikuwa wana wa Daudi, zaidi ya wale kuna wengine aliozaliwa na wahabara yake. Daudi alikuwa na binti vilevile, aliyeitwa Tamari.
10-14Mwana wa Solomono: Rehoboamu,
mwana wa Rehoboamu: Abiya,
mwana wa Abiya: Asa,
mwana wa Asa: Yosafati,
mwana wa Yosafati: Yoramu,
mwana wa Yoramu: Ahazia,
mwana wa Ahazia: Yoasi,
mwana wa Yoasi: Amazia,
mwana wa Amazia: Azaria,
mwana wa Azaria: Yotamu,
mwana wa Yotamu: Ahazi,
mwana wa Ahazi: Hezekia,
mwana wa Hezekia: Manase,
mwana wa Manase: Amoni,
mwana wa Amoni: Yosia.
15Wana wa Yosia walikuwa: Yohana, muzaliwa wake wa kwanza; wa pili Yoyakimu, wa tatu Zedekia na wa ine Salumu.
16Wana wa Yoyakimu walikuwa: Yekonia na Zedekia.
17Wana wa Yekonia, aliyepelekwa kuwa mufungwa na Wababeli, walikuwa: Saltieli,
18Malkiramu, Pedaya, Senazari, Yekamia, Hosama na Nedabia.
19Wana wa Pedaya walikuwa: Zerubabeli na Simei.
Wana wa Zerubabeli walikuwa: Mesulamu na Hanania. Alikuwa na binti mumoja, jina lake Selomiti.
20Zerubabeli vilevile alikuwa na wana wengine watano: Hasuba, Oheli, Berekia, Hasadia na Yusabu-Hesedi.
21Wana wa Hanania walikuwa: Pelatia na Yesaya. Mwana wa Yesaya: Refaya. Mwana wake: Arnani. Mwana wake: Obadia. Mwana wake: Sekania.
22Mwana wa Sekania: Semaya.
Wana wa Semaya walikuwa sita: Hatusi, Igali, Baria, Nearia na Safati.
23Nearia alikuwa na wana watatu: Eliyoenai, Hezekia na Azirikamu.
24Eliyoenai alikuwa na wana saba: Hodavia, Eliasibu, Pelaya, Akubu, Yohana, Dalaya na Anani.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.