1 Mambo ya Siku 3 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wana wa mufalme Daudi

1-3Hawa ndio wana wa mufalme Daudi waliozaliwa wakati alipokuwa kule Hebroni:

Amunoni, muzaliwa wake wa kwanza. Mama yake aliitwa Ahinoamu, wa muji wa Yezereheli;

wa pili: Danieli ambaye mama yake aliitwa Abigaili wa muji wa Karmeli;

wa tatu: Abusaloma, ambaye mama yake aliitwa Maka, binti ya Talmai mufalme wa Gesuri;

wa ine: Adonia, ambaye mama yake aliitwa Hagiti;

wa tano: Sefatia, ambaye mama yake aliitwa Abitali;

wa sita: Itiramu, ambaye mama yake aliitwa Egla.

4Wote sita, walizaliwa Hebroni ambako Daudi alitawala kwa muda wa miaka saba na nusu.

Kule Yerusalema, alitawala kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu.Ang. 2 Sam 5.4,5; 1 Fal 2.11; 1 Sik 29.27

5Hawa ndio wana wa mufalme Daudi waliozaliwa alipokuwa Yerusalema:

Muke wake Bati-Seba, binti ya Amieli, akamuzalia wana wane: Simea, Sobabu, Natani na Solomono.2 Sam 11.3

6Na zaidi ya hao alikuwa na wana wengine tisa: Ibuhari, Elisua, Elifeleti,

7Noga, Nefegi, Yafia,

8Elisama, Eliada na Elifeleti.

9Hao wote walikuwa wana wa Daudi, zaidi ya wale kuna wengine aliozaliwa na wahabara yake. Daudi alikuwa na binti vilevile, aliyeitwa Tamari.

10-14Mwana wa Solomono: Rehoboamu,

mwana wa Rehoboamu: Abiya,

mwana wa Abiya: Asa,

mwana wa Asa: Yosafati,

mwana wa Yosafati: Yoramu,

mwana wa Yoramu: Ahazia,

mwana wa Ahazia: Yoasi,

mwana wa Yoasi: Amazia,

mwana wa Amazia: Azaria,

mwana wa Azaria: Yotamu,

mwana wa Yotamu: Ahazi,

mwana wa Ahazi: Hezekia,

mwana wa Hezekia: Manase,

mwana wa Manase: Amoni,

mwana wa Amoni: Yosia.

15Wana wa Yosia walikuwa: Yohana, muzaliwa wake wa kwanza; wa pili Yoyakimu, wa tatu Zedekia na wa ine Salumu.

16Wana wa Yoyakimu walikuwa: Yekonia na Zedekia.

17Wana wa Yekonia, aliyepelekwa kuwa mufungwa na Wababeli, walikuwa: Saltieli,

18Malkiramu, Pedaya, Senazari, Yekamia, Hosama na Nedabia.

19Wana wa Pedaya walikuwa: Zerubabeli na Simei.

Wana wa Zerubabeli walikuwa: Mesulamu na Hanania. Alikuwa na binti mumoja, jina lake Selomiti.

20Zerubabeli vilevile alikuwa na wana wengine watano: Hasuba, Oheli, Berekia, Hasadia na Yusabu-Hesedi.

21Wana wa Hanania walikuwa: Pelatia na Yesaya. Mwana wa Yesaya: Refaya. Mwana wake: Arnani. Mwana wake: Obadia. Mwana wake: Sekania.

22Mwana wa Sekania: Semaya.

Wana wa Semaya walikuwa sita: Hatusi, Igali, Baria, Nearia na Safati.

23Nearia alikuwa na wana watatu: Eliyoenai, Hezekia na Azirikamu.

24Eliyoenai alikuwa na wana saba: Hodavia, Eliasibu, Pelaya, Akubu, Yohana, Dalaya na Anani.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help