Muhubiri 12 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Ukumbuke Muumba wako

siku za ujana wako

wakati hazijafika siku mbaya

wala haijakaribia miaka utakaposema:

“Sina furaha katika vitu hivyo.”

2Kwa wakati huu wa nyuma,

jua, mwangaza, mwezi na nyota hazionekani tena,

mawingu yanarudia nyuma ya mvua,

3walinzi wa nyumba wanatetemeka,

wenye nguvu wanakunjama,

wasagaji wanaacha kazi kwa sababu ni wachache,

wanaochungulia kwenye dirisha wanakuwa zaifu,

4milango imefungwa,

sauti za visagio zimekuwa ndogo,

watu wanashituliwa na sauti ya ndege,

sauti za muziki zimekuwa ndogo,

5watu wanaogopa mupando

na kutishwa katika njia,

muti wa lozi unachanua maua yake meupe,

mapanzi hayawezi kuruka,

hakuna hamu tena,

mwanadamu anaelekea kwenye makao yake ya milele,

waombolezaji wanasambaa katika njia,

6uzi wa feza unakatika

kikombe cha zahabu kinapondekana,

mutungi wa maji unavunjikia kwenye chemichemi,

gurudumu la kukokota maji linavunjika kwenye kisima,

7mavumbi yanarudilia inchi tena,

na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.

8Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure.

Maneno ya mwisho

9Basi, zaidi ya kuwa na hekima yake, Muhubiri aliendelea kuwafundisha watu ujuzi. Alipima, akachunguza na kutia kwa usawa mezali kwa ufundi mwingi.

10Muhubiri alijikaza kupata maneno ya kupendeza, akaandika kwa usawa maneno ya kweli.

11Misemo ya wenye hekima ni kama fimbo ya kuongoza ngombe. Mezali zilizokusanywa pamoja na muchungaji mumoja ni kama misumari iliyopigiliwa kwa nguvu.

12Zaidi ya hayo, mwana wangu, ujilinde! Kuandika vitabu hakuna mwisho na kusoma kwingi kunachokesha mwili.

13Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.

14Maana, Mungu atahukumu matendo yote, hata yale yanayotendwa kwa siri, yakuwe mazuri au mabaya.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help