1Wakati huo, mufalme Merodaki-Baladani mwana wa Baladani, mufalme wa Babeli, aliposikia kwamba Hezekia alikuwa mugonjwa na sasa amepona, alimutumia wajumbe waliomupelekea barua pamoja na zawadi.
2Basi, Hezekia aliwakaribisha na kuwaonyesha nyumba alimoweka mali yake: feza, zahabu, viungo vya kukoleza chakula, mafuta ya bei kali, vifaa vyake vyote vya vita na vitu vyote vilivyokuwa katika gala zake. Hakuna chochote katika nyumba yake ya kifalme au katika inchi yake ambacho hakuwaonyesha.
3Halafu nabii Isaya alikwenda kwa mufalme Hezekia na kumwuliza: Watu hawa wamesema nini? Na wametoka wapi? Naye Hezekia akamujibu: Wamekuja kutoka inchi ya mbali, kule Babeli.
4Halafu Isaya akamwuliza: Wameona nini katika nyumba yako ya kifalme? Hezekia akamujibu: Wameona yote yanayokuwa katika nyumba yangu ya kifalme. Hakuna chochote katika gala zangu ambacho sikuwaonyesha.
5Halafu Isaya akamwambia Hezekia: Sikia neno la Yawe wa majeshi:
6Siku zinakuja ambapo vyote vinavyokuwa katika nyumba yako na vitu vyote babu zako walivyokusanya mpaka leo, vitapelekwa Babeli. Hakuna kitu chochote kitakachobaki. –Ni Yawe anayesema hivyo.–
7Tena wamoja kati ya watoto wako wanaume watapelekwa, nao watakuwa matowashi watakaotumika katika nyumba ya mufalme wa Babeli. Ang. Dan 1.1–7.2; 2 Fal 24.10-16; 2 Sik 36.10
8Naye Hezekia akamwambia Isaya: Neno la Yawe ulilosema ni zuri. Alisema hivyo maana alifikiri: Kutakuwa amani na salama muda wote wa maisha yangu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.