Ezekieli 7 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Azabu ya mwisho ya Waisraeli

1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

2Wewe mwanadamu, uwaambie wakaaji wa inchi ya Israeli kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Ni Mwisho! Mwisho umeifikia inchi yote, kutoka pande zote ine!

3Sasa mwisho umewafikia;

sasa mutausikia ukali wa hasira yangu juu yenu.

Nitawahukumu kufuatana na mwenendo wenu.

Nitawaazibu kwa ajili ya machukizo yenu yote.

4Sitawaachilia wala sitawaonea huruma.

Nitawaazibu kulingana na mienendo yenu,

nayo machukizo yenu yangali bado kati yenu.

Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.

5Bwana wetu Yawe anasema hivi:

Mutapatwa na hasara! Hasara isiyoonekana bado!

6Mwisho umekuja!

Kweli, mwisho umefika!

Umewafikia ninyi!

7Enyi wakaaji wa inchi hii, maangamizi yenu yamekuja!

Wakati umekuja,

siku imekaribia.

Hiyo ni siku ya makelele

na siyo ya sauti za shangwe kwenye mulima.

8Sasa mutausikia uzito wa hasira yangu juu yenu.

Nitawahukumu kulingana na mwenendo wenu;

nitawaazibu kufuatana na machukizo yenu.

9Sitawaachilia wala sitawaonea huruma.

Nitawaazibu kulingana na mienendo yenu

nayo machukizo yangali bado kati yenu.

Halafu mutatambua kwamba ni mimi Yawe ninayewaangamiza.

10Muangalie, siku ile inakuja!

Maangamizi yenu yamekuja.

Ubaya uko kila pahali na kiburi kimepanda sana.

11Mateso makali yanaendelea kuwa mubaya zaidi.

Hakuna hata mumoja kati yenu atakayebaki,

wala vitu mulivyojilundikia kwa wingi au utajiri wenu;

hakutakuwa mutu mwenye heshima kati yenu.

12Wakati umetimia,

ile siku imekaribia.

Mununuzi asifurahi wala muchuuzi asiomboleze;

kwa sababu kasirani yangu itawaangukia watu wote.

13Wachuuzi watahomba kabisa

hata ikiwa wangali wazima.

Kwa maana unabii huu ni juu ya watu wote nao hautavunjwa.

Kutokana na uovu wake, mutu hatayaokoa maisha yake.

14Baragumu imepigwa na kuwafanya wote wakuwe tayari.

Lakini hakuna anayekwenda kwa vita,

kwa maana kasirani yangu iko juu ya watu wote.

15Inje kuna kifo kwa upanga

na ndani ya muji kuna ugonjwa mukali na njaa.

Wanaokuwa katika vijiji watakufa kwa upanga;

wanaokuwa katika muji wataangamizwa na njaa na ugonjwa mukali.

16Ikiwa kuna watu walioponyoka,

watakimbilia kwenye milima kama njiwa waliotishwa katika bonde.

Kila mumoja wao ataomboleza kwa ajili ya zambi zake.

17Mikono ya kila mutu itakuwa zaifu

na magoti yake yataregea kabisa.

18Watavaa gunia,

hofu itawashika,

nao watapata haya na vichwa vyao vyote vitanyolewa.

19Watatupa feza yao ndani ya barabara

na zahabu yao itakuwa kama kitu kichafu.

Feza na zahabu zao hazitaweza kuwaokoa

katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe;

wala hawataweza kushiba

au kujaza tumbo zao feza na zahabu waliyojilundikia;

maana mali hiyo ndiyo iliyosababisha zambi yao.

20Walijivuna kwa ajili ya vitu vyao vizuri vya mapambo,

wakajifanyia sanamu za miungu zinazochukiza,

vitu vibaya kabisa.

Kwa sababu hiyo nitavifanya kuwa uchafu mbele yao.

21Utajiri wao nitautia katika mikono ya mataifa mengine;

watu waovu wa dunia wataunyanganya na kuuchafua.

22Nitageuza uso wangu usiwaelekee;

nitaachilia hekalu langu lichafuliwe.

Wanyanganyi wataingia humo ndani na kulichafua.

23Tengeneza munyororo;

kwa maana inchi imejaa makosa ya umwangaji wa damu

na muji umejaa mateso makali.

24Nitaleta watu wa mataifa mabaya sana

nao watarizi nyumba zao.

Nitakikomesha kiburi chao,

na pahali pao pa kutambikia patachafuliwa.

25Uchungu mukali utakapowafikia,

watatafuta amani, lakini haitapatikana.

26Watapata hasara kwa mufululizo;

nazo habari mbaya zitafuatana.

Watamwomba nabii awatabirie.

Makuhani hawatakuwa na sheria yoyote;

na wazee watakosa shauri la kuwapatia.

27Mufalme ataomboleza,

mukubwa atakata tamaa

na watu watatetemeka kwa hofu.

Nitawatendea kufuatana na mienendo yao,

nitawahukumu kama nilivyowahukumu wengine.

Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help