1 Wafalme 3 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Solomono anaomba hekima(2 Sik 1.3-12)

1Solomono alifanya mapatano na mufalme wa Misri, kwa kumwoa binti yake. Akamuleta binti wa mufalme wa Misri na kumuweka katika muji wa Daudi, mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake mwenyewe, nyumba ya Yawe, na ukuta wa kuuzunguka Yerusalema.

2Kwa wakati ule, watu walikuwa wakitoa sadaka kule juu ya vilima, kwa kuwa nyumba ya Mungu ilikuwa bado haijajengwa.

3Solomono alimupenda Yawe, akashika masharti ya baba yake Daudi; lakini tu, naye alitoa sadaka na kufukiza ubani juu ya vilima.

4Wakati mumoja, Solomono alikwenda kutoa sadaka kule kwenye kilima cha Gibeoni, maana palikuwa ndipo pahali pakubwa pa ibada. Ilikuwa ni kawaida ya Solomono kutoa maelfu ya sadaka za kuteketezwa katika mazabahu hiyo.

5Kule Gibeoni, Yawe alimutokea Solomono katika ndoto usiku, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka nami nitakupa.”

6Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.

7Ee Yawe, Mungu wangu, umeniweka mimi mutumishi wako kuwa mufalme pahali pa baba yangu Daudi, ijapokuwa ningali mutoto mudogo na sijui namna ya kutimiza kazi hii.

8Na hapa umeniweka kati ya watu wako ambao umewachagua; nao ni wengi hata hawawezi kuhesabika kwa sababu ya wingi wao.

9Kwa hiyo, ninakuomba unipe mimi mutumishi wako moyo wa hekima nipate kuamua watu wako, niweze kutambua mazuri na mabaya; maana ni nani anayeweza kuhukumu watu wako wanaokuwa wengi hivi?”

10Ombi hili la Solomono lilimufurahisha Yawe,

11naye akamwambia: “Kwa sababu umetoa ombi hili, na haukujiombea maisha marefu au mali, na wala haukuomba waadui zako waangamizwe, lakini umejiombea hekima ya kutoa hukumu au kutenda haki,

12basi, sasa ninakutimizia kama ulivyoomba. Ninakupa hekima na akili kwa kipimo ambacho hakuna mutu mwingine aliyepata kuwa nacho mbele yako, na wala hakutatokea mwingine kama wewe nyuma yako.

13Vilevile, nitakupa yale ambayo haukuomba: nitakupa utajiri na heshima zaidi ya mufalme mwingine yeyote wa nyakati zako.

14Tena kama ukifuata njia yangu na kushika masharti na amri zangu kama vile baba yako Daudi alivyofanya, basi, nitakupa maisha marefu.”

15Solomono alipoamuka, alitambua kwamba ilikuwa ndoto. Halafu akarudi Yerusalema, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Yawe, akamutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Halafu akawafanyia watumishi wake wote karamu.

Solomono anaamua maneno magumu

16Siku moja, wanawake wawili wakahaba walikwenda kwa mufalme Solomono.

17Mumoja wao akasema: “Ee bwana wangu, mimi na huyu mwenzangu tunakaa nyumba moja. Mimi nilizaa mutoto mwanaume huyu akiwa pale.

18Nyuma ya siku tatu huyu naye akazaa mutoto mwanaume. Hakukukuwa mutu mwingine ndani ya nyumba isipokuwa sisi wawili tu.

19Halafu, usiku mumoja, mutoto wake akakufa kwa sababu alimulalia.

20Kisha akaamuka usiku kati, akamutwaa mwana wangu kutoka kwangu wakati mimi niko katika usingizi, akamulalisha kwenye kufua chake. Halafu akatwaa maiti ya mwana wake, akailalisha kwenye kifua changu.

21Nilipoamuka asubui na kutaka kumunyonyesha mwana wangu, nikakuta mutoto amekufa. Nilipochunguza sana, nikagundua kwamba hakukuwa mwana wangu niliyemuzaa.”

22Lakini yule mwanamuke mwingine akasema: “Hapana! Wa kwangu ndiye anayekuwa muzima na wa kwako ndiye aliyekufa”.

Naye mwanamuke wa kwanza akasema: “Hapana! Mutoto wako ndiye aliyekufa, wangu ni huyo anayekuwa muzima!” Basi, wakaendelea kubishana hivyo mbele ya mufalme.

23Halafu mufalme Solomono akasema: “Kila mumoja wenu anadai kwamba mutoto wake ndiye mwenye kuwa muzima na kwamba aliyekufa si wake.”

24Basi, mufalme akaagiza: “Muniletee upanga!” Wakamuletea mufalme upanga.

25Mufalme akasema: “Mukate huyo mutoto muzima vipande viwili, uwape wamama hawa kila mumoja nusu ya mutoto.”

26Yule mwanamuke aliyekuwa mama ya huyo mutoto anayekuwa muzima alishikwa na huruma juu ya mwana wake, akamwambia mufalme: “Tafazali mufalme, musimwue mutoto. Mumupe mwenzangu huyo mutoto mwenye kuwa muzima, amutwae yeye.”

Lakini yule mwanamuke mwingine akasema: “Hapana! Mutoto asikuwe wangu wala wake. Mumukate vipande viwili.”

27Mufalme Solomono akasema: “Usimwue mutoto! Umupe mwanamuke wa kwanza amutwae, maana yeye ndiye mama yake.”

28Watu wote wa Israeli waliposikia juu ya hukumu ya mufalme, walimwogopa. Wakatambua kwamba alikuwa na hekima ya Mungu iliyomuwezesha kutoa hukumu za haki.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help