1Wana wangu, musikilize maadibisho ya baba yenu,
mutege sikio mupate kuwa na akili.
2Maana ninawapa kanuni zuri,
musikatae mafundisho yangu.
3Mimi vilevile nilikuwa mutoto kwa baba yangu,
nilikuwa mupole, kipenzi cha mama yangu.
4Baba yangu alinifundisha hiki:
“Shika kwa moyo maneno yangu,
shika amri zangu nawe utaishi.
5Ujipatie hekima, ujipatie ufahamu;
usisahau wala kuzarau maneno yangu.
6Usimwache hekima, nayo itakutunza;
umupende, nayo itakulinda.
7Jambo la musingi ni kujipatia hekima;
toa vyote unavyokuwa navyo ujipatie akili.
8Shikamana sana na hekima, nayo itakutukuza;
ukiishikilia itakupa heshima.
9Itavalisha kilemba cha neema kwenye kichwa chako,
atakupa taji lenye utukufu.”
10Mwana wangu, sikia na kupokea maneno yangu,
kusudi upate kuwa na miaka mingi ya kuishi.
11Nimekufundisha njia ya hekima,
nimekuongoza katika njia ya usawa.
12Ukitembea hatua zako hazitazuizwa,
wala ukikimbia hautajikwaa.
13Shika mafundisho ya hekima na usimwache iponyoke,
uishike kwa uangalifu maana ni uzima wako.
14Usijiingize katika njia ya waovu,
wala usifuate mwenendo wa watu wabaya.
15Epuka njia hiyo wala usiikaribie;
ujiepushe nayo, uende zako.
16Waovu hawalali hata kidogo wasipotenda uovu;
hawapati usingizi wasipomukwaza mutu.
17Maana uovu ndicho chakula chao,
mateso makali ndiyo divai yao.
18Njia ya wenye haki ni kama mwangaza wa asubui mapema,
ambao unaangaza zaidi na zaidi hata muchana kamili.
19Lakini njia ya waovu ni kama giza nene,
hawajui kinachowafanya wajikwae.
20Mwana wangu, sikia kwa uangalifu maneno yangu,
utegee sikio masemi yangu.
21Usiyaache yatoweke mbele ya macho,
uyafunge ndani ya moyo wako.
22Maana hayo ni uzima kwa mutu anayeyapata,
ni dawa kwa mwili wake wote.
23Linda moyo wako kwa uangalifu wote,
maana mule munatokea chemichemi za uzima.
24Tenga mbali nawe luga potovu;
wala midomo yako isiseme maneno madanganyifu.
25Uyaelekeze macho yako mbele sawasawa,
kope zako zipige sawasawa.
26Chunguza sana njia utakayopitia,
na hatua zako zote zitakuwa kamili.
27Usigeukie kuume wala kushoto;
epusha muguu wako mbali na uovu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.