1Kisha nikaona kwamba katika lile anga juu ya vichwa vya makerubi kulikuwa kitu kinachofanana na jiwe la rangi ya samawi, umbo lake kama kiti cha kifalme.
3Wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa nyumba ya Yawe, yule mutu alipoingia ndani; wingu likafunika kiwanja cha ndani.
4Utukufu wa Yawe ukapanda juu tokea wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha nyumba hiyo, na lile wingu likaijaza nyumba, na kiwanja kilijaa mwangaza wa utukufu wa Yawe.
5Shindo la mabawa ya makerubi iliweza kusikilika hata kwenye kiwanja cha inje, kama sauti ya Yawe wa majeshi anaposema.
6Yawe alipomwamuru yule mutu aliyevaa nguo ya kitani atwae moto toka katikati ya magurudumu yaliyokuwa chini ya makerubi, yule mutu alikwenda na kusimama pembeni ya gurudumu moja.
7Kerubi mumoja akanyoosha mukono wake kwa kutwaa moto uliokuwa katikati ya makerubi, akatwaa sehemu yake na kuutia katika mikono ya yule mutu aliyevaa nguo ya kitani; naye alipoupokea, akajiendea.
8Makerubi hao walionekana kuwa na kitu kama mukono wa mutu chini ya mabawa yao.
9Niliangalia, nikaona kulikuwa magurudumu mane, gurudumu moja pembeni ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama jiwe la zabarajadi. Ang. Eze 1.15-21
10Yote mane yalionekana kuwa ya namna moja, na kila gurudumu lilionekana kama liko ndani ya gurudumu lingine.
11Yaliweza kwenda pande zote bila kugeuka; kule gurudumu la kwanza lilielekea, yote yalifuata.
12Miili ya hao makerubi, migongo yao, mikono na mabawa yao, pamoja na magurudumu, vyote vilijaa macho pande zote. Ang. Ufu 4.8
13Niliambiwa kwamba magurudumu yale yanaitwa “Magurudumu Yanayozunguka”.
14Kila kerubi alikuwa na nyuso ine: uso wa kwanza ulikuwa wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa ine ulikuwa wa tai. Ang. Eze 1.10; Ufu 4.7
15Makerubi wakanyanyuka juu. Hawa ndio vile viumbe niliowaona karibu na muto Kebari.
16Makerubi wale walipokwenda, magurudumu nayo yalikwenda pembeni yao. Walipokunjua mabawa yao kusudi wapande juu, magurudumu nayo yalikwenda pamoja nao.
17Waliposimama, magurudumu nayo yalisimama; hao walipopanda juu, magurudumu nayo yalipanda pamoja nao. Maana roho wa hao viumbe ilikuwa katika magurudumu hayo.
18Kisha utukufu wa Yawe ulitoka kwenye kizingiti cha nyumba, ukaenda na kusimama juu ya wale makerubi.
19Makerubi wakakunjua mabawa yao, wakapanda juu, mimi nikiwa ninawaona na yale magurudumu yalikuwa pembeni yao. Wakasimama mbele ya mulango wa upande wa mashariki wa nyumba ya Yawe, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
20Hawa walikuwa wale viumbe niliowaona chini ya Mungu wa Israeli karibu na muto Kebari, nami nikatambua kwamba ni makerubi.
21Kila mumoja wao alikuwa na nyuso ine na mabawa mane na chini ya kila bawa kulikuwa kitu kinachokuwa kama mukono wa mutu.
22Vilevile nilizitambua nyuso zao: zilikuwa zilezile nilizokuwa nimeziona kule kwenye muto Kebari. Kila kiumbe kilikwenda mbele, moja kwa moja.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.