1Maombi ya Daudi.
Unitegee sikio,
ee Yawe,
unijibu,
maana mimi ni masikini na mukosefu.
2Ulinde maisha yangu maana mimi ni mwaminifu mbele yako;
uniokoe mimi mutumishi wako ninayekutegemea.
3Wewe ni Mungu wangu;
basi, unionee huruma,
maana ninakulilia muchana kutwa.
4Ee Bwana wetu, ninakutolea moyo wangu.
Ufurahishe roho yangu mimi mutumishi wako.
5Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe,
mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.
6Ee Yawe, utegee maombi yangu sikio;
usikilize kilio cha ombi langu.
7Siku za taabu ninakuita,
maana wewe unaniitikia.
8Ee Bwana, hakuna mungu mwingine anayekuwa kama wewe;
hakuna anayeweza kufanya unayofanya wewe.
9Mataifa yote uliyoumba, yatakuja kukuabudu, ee Bwana;
yatatangaza ukubwa wa jina lako.
10Wewe ndiwe mukubwa, unafanya maajabu;
wewe peke yako ndiwe Mungu.
11Unifundishe njia yako, ee Yawe,
nipate kuwa mwaminifu kwako;
uongoze moyo wangu nikuheshimu.
12Ee Bwana, Mungu wangu, nitakusifu kwa moyo wote;
nitatangaza ukubwa wa jina lako milele.
13Wema wako kwangu ni mwingi sana!
Umeniokoa kutoka katika kuzimu.
14Ee Mungu, watu wenye kiburi wamenishambulia;
kundi la watu wakali lilitaka kuniua,
wala halikujali wewe hata kidogo.
15Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma;
wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.
16Unigeukie, unihurumie;
unijalie nguvu yako mimi mutumishi wako,
umwokoe mutoto wa mujakazi wako.
17Unionyeshe kitambulisho cha wema wako, ee Yawe,
kusudi wale wanaonichukia wafezeheke,
wanapoona umenisaidia na kunifariji.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.