1Kutoka Mukubwa wa Wakora. Zaburi ya Wakora.
2Enyi watu wote, mupige vigelegele!
Mumusifu Mungu kwa sauti za shangwe!
3Maana Yawe, Mungu Mukubwa, anaogopesha.
Yeye ni mufalme mukubwa wa ulimwengu wote.
4Ametuwezesha kuwashinda watu wa mataifa,
ameyaweka mataifa chini ya mamlaka yetu.
5Ametuchagulia inchi hii ikuwe urizi wetu,
ambayo ni utukufu wa Yakobo anayemupenda.
6Mungu anapanda kwenye kiti chake cha kifalme,
anashangiliwa na kupigiwa baragumu.
7Mumwimbie Mungu sifa, mumwimbie!
Mumwimbie mufalme wetu sifa, mumwimbie!
8Mumwimbie Mungu mashairi ya sifa;
maana yeye ni mufalme wa ulimwengu wote.
9Mungu anatawala mataifa yote;
ameikaa katika kiti chake kitakatifu cha kifalme.
10Waongozi wa mataifa wanakusanyika,
wanajiunga na watu wa Mungu wa Abrahamu,
maana watawala wa dunia wako chini ya Mungu,
yeye ni juu ya yote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.