1Mufuate tabia ya Mungu kwa maana ninyi ni watoto wake wapendwa.
2Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.
3Kama vile inavyowapasa watu wa Mungu kuishi, tendo lolote la uasherati, la uchafu wala la tamaa ya mali lisisikilike kati yenu.
4Vilevile kusisikilike maneno ya matusi ya ovyo ovyo wala machafu, kwa maana hayana mafaa. Kinachofaa ni kumushukuru Mungu.
5Mujue waziwazi kwamba mwasherati yeyote na muchafu na mwenye tamaa ya mali (mwenye tamaa ni kama mwenye kuabudu sanamu), hao wote hawatapewa sehemu ya urizi katika Ufalme wa Kristo na Mungu.
6Mutu asiwadanganye na maneno yasiyokuwa na maana; kwa sababu ya makosa kama hayo, Mungu anawaazibu kwa kasirani yake wale wasiomutii.
7Basi musishirikiane na watu kama wale.
8Zamani muliishi katika giza, lakini sasa, kwa kuungana kwenu na Bwana, munaishi katika mwangaza. Muishi kama watoto wa mwangaza,
9kwa maana matunda ya mwangaza ni wema wa kila namna, haki na ukweli.
10Mujikaze kutambua mambo yanayomupendeza Bwana.
11Musishiriki katika matendo ya giza yasiyofaa, lakini muyafichue.
12(Kwa maana ni haya kusema juu ya mambo watu hao wanayofanya kwa siri.)
13Lakini matendo yale yote yanapofunuliwa katika mwangaza, yanaonekana wazi.
14Kwa maana yote yanayoonekana wazi yanageuka mwangaza. Ni kwa hiyo inasemwa hivi:
“Amuka wewe unayelala!
Ufufuke kutoka kati ya wafu,
naye Kristo atakuangazia.”
15Muangalie vizuri mwenendo wenu. Musiishi kama wajinga lakini muishi kama wenye hekima.
16Mutumie vema wakati huu munaokuwa nao kwa maana siku hizi ni mbaya.
17Kwa hiyo musikuwe wajinga, lakini mutambue mapenzi ya Bwana.
18Musilewe divai kwa maana inaleta upotovu, lakini mujazwe na Roho.
19Munapoongea, museme maneno ya zaburi, mumusifu Bwana na kumwabudu kwa nyimbo za kiroho. Mumwimbie na kumushangilia kwa moyo wenu wote.
20Mumushukuru Mungu Baba siku zote kwa kila jambo, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
Maonyo kwa wake na waume21Mukuwe na utii ninyi kwa ninyi kwa kumuheshimu Kristo.
22Wake wawatii waume wao kama vile wanavyomutii Bwana.
23Kwa maana mume ni kichwa cha muke wake, kama vile Kristo anavyokuwa kichwa cha kanisa. Naye mwenyewe ni Mwokozi wa kanisa ambalo ni mwili wake.
24Wake wanapaswa kutii waume wao katika kila jambo sawa vile kanisa linavyomutii Kristo.
25Nanyi waume muwapende wake wenu sawa vile Kristo alivyopenda kanisa na kutoa uzima wake kwa ajili yake.
26Alifanya hivi kusudi atakase kanisa kwa ajili ya Mungu, akilisafisha kwa maji na kwa neno.
27Alitaka hivi kujipatia yeye mwenyewe kanisa tukufu na takatifu, lisilokuwa na taka wala kikunjo wala kilema chochote.
28Hivi vilevile waume wanapaswa kupenda wake wao kama vile wanavyopenda miili yao wenyewe. Yule anayependa muke wake, anajipenda yeye mwenyewe.
29Kwa maana hakuna mutu anayeweza kuchukia mwili wake mwenyewe, lakini anaukulisha na kuuchunga kama Kristo anavyotendea kanisa,
30kwa sababu sisi ni viungo vya mwili wake.
31Ni sawasawa inavyosemwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu hii, mume ataacha baba yake na mama yake na kuungana na muke wake, nao wawili watakuwa mwili mumoja.”
32Ni vigumu sana kuelewa siri hii, lakini ninasema mambo yanayoelekea Kristo na kanisa.
33Ingawa hivi, kwa ngambo yenu vilevile, kila mume anapaswa kumupenda muke wake kama vile anavyojipenda, na kila muke anapaswa kuheshimu mume wake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.