Isaya 33 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Hasara kwa mwangamizaji

1Ole kwako!

Unaangamiza ingawa hauangamizwi.

Unadanganya ingawa haudanganywi.

Utakapokwisha kuangamiza,

wewe utaangamizwa!

Utakapomaliza kudanganya,

wewe utadanganywa.

2Ee Yawe, utuonee huruma,

kwako tumeliweka tumaini letu.

Ukuwe kikingio chetu kila siku,

mwokozi wetu wakati wa taabu.

3Kwa kishindo cha sauti yako watu wanakimbia;

unaposimama tu, mataifa yanatawanyika.

4Waadui zao wanakusanya vitu walivyonyanganya,

wanavirukia kama mapanzi.

5Yawe ametukuzwa,

yeye anaishi juu mbinguni.

Ameujaza Sayuni usawa na haki.

6Enyi watu wa Yerusalema,

Yawe atawajalia usalama,

atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa.

Akiba yenu kubwa ni kumwogopa Yawe.

7Muangalie, washujaa wao wanalia,

wajumbe wa amani wanaomboleza.

8Barabara kubwa zimebaki tupu;

hakuna anayesafiri kupitia ndani yao.

Mapatano yanavunjwa ovyo,

washuhuda wanazarauliwa.

Hakuna anayejali tena maisha ya wanadamu.

9Inchi inaomboleza na kunyauka;

pori ya Lebanoni imekauka,

bonde zuri la Saroni limekuwa jangwa,

kule Basani na mulima Karmeli

majani yote yamekauka.

Yawe anawaonya waadui zake

10Yawe anasema hivi:

Sasa mimi nitasimama;

sasa nitajiweka tayari;

sasa mimi nitatukuzwa.

11Mipango yenu yote ni kama maganda,

na matokeo yake ni takataka tupu.

Pumzi yangu itawaangamiza kama moto.

12Watu watakuwa kama wamechomwa kuwa majivu,

kama miiba iliyokatwa na kuteketezwa katika moto.

13Musikilize mambo muliyofanya, enyi munaokuwa mbali;

nanyi munaokuwa karibu, mutambue uwezo wangu.

14Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa,

wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema:

Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali?

Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?

15Ni mutu anayekuwa hivi:

anaishi kwa haki na kusema kwa usawa,

anazarau kabisa utajiri wa unyanganyi,

anakataa kupokea kituliro,

hakubali hata kidogo kusikia mipango ya mauaji,

wala hakubali macho yake yaone maovu.

16Mutu wa namna hiyo anaishi kwenye nafasi ya juu,

pahali salama, penye pango na mawe makubwa;

atapewa chakula chake siku zote,

na maji yake ya kunywa hayatakosekana.

Wakati muzuri unaokuja

17Mutaweza kumwona mufalme katika utukufu wake,

mutaiona inchi anayotawala, kubwa na pana.

18Mutakumbuka kitisho kilichopita na kujiuliza:

Wako wapi wale waliokadirisha na kuchunguza kodi?

Wako wapi wale waliopeleleza ugumu wa kuta zetu?

19Hamutawaona tena watu wale wenye kiburi,

wanaozungumuza luga isiyoeleweka.

20Muangalie Sayuni tunamofanyia sikukuu zetu;

muangalie Yerusalema, makao matulivu, hema imara;

misumari yake haitaongolewa hata kidogo,

kamba zake hazitakatwa hata moja.

21Humo Yawe atatuonyesha ukubwa wake.

Kutakuwa mito mikubwa na vijito,

lakini mashua za vita hazitapita,

wala mashua kubwa kuingia.

22Maana Yawe ni mwamuzi wetu,

yeye ni mutawala wetu;

Yawe ni mufalme wetu,

yeye ndiye anayetuokoa.

23Ewe Sayuni, kamba zako zimeregea,

haziwezi kushikilia matanga yake,

wala kufungia paa zao.

Lakini vitu vingi vilivyonyanganywa vitagawanywa;

hata vilema wataweza kupata sehemu yao.

24Hakuna atakayesema tena ni mugonjwa;

watu watasamehewa uovu wao wote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help