Zaburi 14 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Uovu wa watu(Ang. Zab 53)

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.

Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo:

“Hakuna Mungu.”

Wote wamepotoka kabisa,

matendo yao ni ya kuchukiza;

hakuna hata mumoja anayetenda mazuri!

2Yawe anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni

aone kama kuna yeyote mwenye akili,

kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.

3Lakini wote wamekosa,

wote wamepotoka pamoja;

hakuna anayetenda mazuri,

hakuna hata mumoja.

4Hao wanaotenda maovu hawajui kitu?

Wanatafuna watu wangu kama mikate,

wala hawajali Yawe.

5Hapo watashikwa na hofu,

maana Mungu ni pamoja na watu wa haki.

6Unaweza kuvuruga mipango ya masikini,

lakini Yawe ndiye kimbilio lake.

7Heri ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Sayuni!

Yawe atakapotengeneza hali ya watu wake,

wazao wa Yakobo watashangilia;

watu wa Israeli watafurahi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help