1Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.
2Hii ndiyo namna tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu: kwa kumupenda Mungu na kushika amri zake.
3Kwa maana kumupenda Mungu ni kutii amri zake. Na amri zake si ngumu,
4kwa sababu kila mutoto wa Mungu anashinda dunia. Tunashinda dunia kwa njia ya imani yetu.
5Ni nani anayeshinda dunia? Ni yule anayeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
Ushuhuda juu ya Yesu Kristo6Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji ya ubatizo wake na kwa damu ya kufa kwake. Hakukuja na maji tu, lakini pamoja na maji na damu. Naye Roho ndiye anayeshuhudia mambo yale kwa sababu Roho ni wa ukweli.
7Maana kuna washuhuda watatu:
8Roho, maji na damu, nao watatu wanapatana kwa ushuhuda mumoja.
9Kama tunakubali ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni wenye maana zaidi, na ni huu ndio ushuhuda Mungu aliotoa juu ya Mwana wake.
10Yule anayemwamini Mwana wa Mungu yuko na ushuhuda huu ndani yake. Lakini yule asiyemwamini Mungu, amemufanya Mungu kuwa mwongo, maana hakuaminia ushuhuda Mungu aliotoa juu ya Mwana wake.
11Na huu ndio ushuhuda ule: Mungu alitupatia uzima wa milele na uzima huu unapatikana kwa njia ya Mwana wake.
12Yule anayekuwa na Mwana wa Mungu yuko na uzima ule, lakini yule asiyekuwa na Mwana wa Mungu hana uzima.
Uzima wa milele13Ninawaandikia maneno yale, ninyi wenye kuamini kwa jina la Mwana wa Mungu, mupate kujua kwamba muko na uzima wa milele.
14Nasi tuko na tumaini hili mbele ya Mungu: tunajua kwamba atatusikiliza tukimwomba kitu chochote kufuatana na mapenzi yake.
15Basi, ikiwa tunajua kwamba anatusikiliza wakati tunapomwomba, tunajua vilevile kwamba anatupatia chochote tulichomwomba.
16Mutu akimwona ndugu yake anafanya zambi isiyoleta kifo, anapaswa kumwombea kwa Mungu, Mungu atamupa mutu yule uzima. Jambo hili linaelekea wale wanaotenda zambi isiyoleta kifo. Maana kuna zambi inayoleta kifo lakini sisemi kama ataomba juu ya hiyo.
17Kila tendo lisilokuwa la haki ni zambi, lakini kuna zambi isiyoleta kifo.
18Tunajua kwamba kila mutoto wa Mungu hafanyi zambi, kwa maana Mwana wa Mungu anamulinda, wala yule Mwovu hawezi kumugusa.
19Tunajua kwamba sisi ni watoto wa Mungu ingawa dunia yote inatawaliwa na yule Mwovu.
20Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.
21Watoto wangu wapendwa, muepuke kuabudu sanamu za miungu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.