1“Kisha Yawe akaniambia: ‘Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, na sanduku la mbao. Kuja kwangu huku juu kwenye mulima,
2nami nitaandika maneno yaliyokuwa yameandikwa katika vibao vile ulivyovunja, kisha uweke vibao hivyo katika sanduku’.
3“Basi, nikatengeneza sanduku la mushita na vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nikavitwaa katika mukono, nikapanda navyo kwenye mulima.
4Yawe akaandika katika vibao hivyo maneno kama yaleyale ya kwanza: amri kumi ambazo aliwapa aliposema kutoka katika moto siku ya mukutano. Halafu Yawe akanipa vibao hivyo.
5Nikageuka, nikashuka kutoka kwenye mulima, nikaweka vibao hivyo ndani ya sanduku nililokuwa nimetengeneza, na vimo ndani ya sanduku hilo, kama vile Yawe alivyoniamuru.”
6(Watu wa Israeli wakasafiri kutoka visima vya watu wa Yakani mpaka Musara. Haruni akakufa na kuzikwa kule. Eleazari mwana wake, akatwaa nafasi yake kama vile kuhani.
7Kutoka pale, wakasafiri mpaka Gudigoda, na kutoka Gudigoda mpaka Yotibata, eneo lenye vijito vingi vya maji.
8Wakati huo, Yawe akachagua watu wa kabila la Lawi wakuwe wanabeba Sanduku la Agano la Yawe, wamutumikie kama vile makuhani na kubariki watu kwa jina lake hata hivi leo.
9Ndiyo maana kabila la watu wa Lawi halina sehemu ya inchi ya urizi pamoja na wandugu zao. Walichopokea ni heshima ya kuwa makuhani wa Yawe, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyoahidi.)
10“Nikakaa kwenye mulima kwa muda wa siku makumi ine, usiku na muchana, kama vile mbele. Yawe akanisikiliza kwa mara ingine tena na akakubali kutowaangamiza.
11Kisha akaniambia: ‘Ondoka uendelee na safari yako ukiwaongoza watu kusudi waweze kuingia na kurizi inchi niliyowaapia babu zenu kwamba nitawapa’.
Kitu Mungu anachotaka12“Sasa, enyi Waisraeli, Yawe, Mungu wenu, anataka nini kwenu? Yawe, Mungu wenu, anataka mumwogope, mufuate njia zake zote, mumupende, mumutumikie Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wote na kwa roho yenu yote,
13na mutii amri na masharti ya Yawe ninayowawekea leo, kwa mafaa yenu wenyewe.
14Angalia, mbingu hata mbingu za mbingu ni mali ya Yawe, Mungu wenu, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake.
15Tena Yawe alifurahia babu zenu kwa kuwapenda na akawachagua ninyi wazao wao pahali pa watu wengine wote, kama hivi leo.
16Kwa hiyo, mutahiri magovi ya mioyo yenu, musikuwe wagumu tena.
17Maana Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa wabwana. Yeye ni Mungu mukubwa na mwenye nguvu, na wa kuogopesha. Hapendelei wala hapokei kituliro.
18Anatetea haki ya wayatima na wajane; vilevile anawapenda wageni na kuwapa chakula na nguo.
19Basi, muwapende wageni kwa sababu nanyi vilevile mulikuwa wageni katika inchi ya Misri.
20Mumwogope Yawe, Mungu wenu, mumutumikie, muambatane naye na kuapa kwa jina lake.
21Yeye ni utukufu wenu. Yeye ni Mungu wenu ambaye amewatendea haya mambo makubwa na ya kutisha muliyoona kwa macho yenu wenyewe.
22Babu zenu walipokwenda Misri, walikuwa watu makumi saba tu, lakini sasa Yawe, Mungu wenu, amewafanya kuwa wengi kama nyota mbinguni.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.