1Siku moja, Samusoni aliteremuka na kwenda Timuna ambako alimwona binti mumoja Mufilistini.
2Aliporudi kwa nyumba akawaambia wazazi wake: “Nimemwona binti mumoja Mufilistini kule Timuna. Munioee binti huyo.”
3Lakini wazazi wake wakamwambia: “Hakuna binti yeyote kati ya wandugu zako au kati ya watu wetu kusudi uende kuoa kwa Wafilistini wasiotahiriwa?”
Lakini Samusoni akamwambia baba yake: “Munioee binti huyo, maana ananipendeza sana.”
4Wazazi wake hawakujua kwamba ule ulikuwa mupango wa Yawe ambaye alikuwa anatafuta njia ya kushambulia Wafilistini. Wakati ule, Wafilistini walikuwa wakiwatawala Waisraeli.
5Samusoni na wazazi wake wakaondoka kwenda Timuna. Walipofika kule kwenye mashamba ya mizabibu, simba mukali mumoja akatokea akamungurumia Samusoni.
6Basi, roho wa Yawe akamushika Samusoni kwa nguvu, akamurarua simba huyo kama mutu anavyorarua mwana-mbuzi. Naye Samusoni hakuwaambia wazazi wake jambo lile.
7Kisha akateremuka akaenda kuzungumuza na yule binti. Yule binti alimupendeza sana Samusoni.
8Nyuma ya siku chache akarudi kule Timuna kwa kumutwaa yule binti. Alipokuwa katika njia akageuka pembeni kwa kuangalia muzoga wa yule simba, kumbe kulikuwa nyuki na asali ndani ya muzoga.
9Basi, akapakua asali kwa mikono yake, akaikula akiendelea na safari yake. Aliporudi kwa wazazi wake, akawapa asali kidogo nao wakakula. Lakini hakuwaambia kwamba alitosha asali hiyo ndani ya muzoga wa simba.
10Baba yake akaenda katika nyumba ya yule binti, naye Samusoni akafanya karamu kule, kama vile vijana walivyofanya kwa wakati ule.
11Wafilistini walipomwona Samusoni wakamuletea vijana makumi tatu wakae naye.
12Samusoni akawaambia: “Nitatega kitendawili. Kama mukiweza kutegua kitendawili hicho kwa muda wa siku saba za sherehe za arusi, basi, nitawapa nguo makumi tatu za kitani na nguo makumi tatu za sikukuu.
13Lakini musipoweza kukitegua, ninyi mutanipa nguo makumi tatu za kitani na nguo makumi tatu za sikukuu.”
14Nao wakamwambia: “Sasa tega tusikie.”
Samusoni akawaambia:
“Katika mwenye kula kukatoka chakula
na katika mwenye nguvu kukatoka utamu.”
Nyuma ya siku tatu hao vijana walikuwa bado hawajaweza kutegua hicho kitendawili.
15Basi siku ya ine wakamwambia muke wa Samusoni: “Umubembeleze mume wako kusudi atuambie maana ya kitendawili hicho, kama sivyo tutakuteketeza kwa moto wewe pamoja na nyumba ya baba yako. Ninyi mulitualika hapa kutunyanganya mali zetu?”
16Muke wa Samusoni akamwendea Samusoni, na machozi yakimutiririka, akamwambia: “Kwa kweli unanichukia; haunipendi hata kidogo. Umewategea kitendawili watu wangu na haukuniambia maana yake.”
Samusoni akamujibu: “Mimi sijawaelezea hata wazazi wangu. Sasa nitaweza namna gani kukuelezea wewe?”
17Lakini aliendelea kulia katika muda wao wote wa siku saba za sherehe za arusi. Siku ya saba Samusoni akamwambia muke wake kile kitendawili kwa sababu alimwuzi sana. Muke wake akaenda haraka akawaambia watu wake.
18Siku hiyo ya saba, mbele ya jua kutua, wakamwambia Samusoni,
“Ni kitu gani kitamu kuliko asali?
Ni nani mwenye nguvu kuliko simba?”
Samusoni akawajibu: “Kama hamungejishugulisha na mwana-ngombe wangu hamungeweza kukitegua kitendawili changu.”
19Hapo roho wa Yawe akamushika Samusoni kwa nguvu, naye akaenda muji Askeloni, akawaua watu makumi tatu, kisha akatwaa nguo zao za sikukuu, akawapa wale waliotegua kitendawili chake. Halafu akaondoka, akaenda kwa nyumba kwa wazazi wake akiwa na hasira kali.
20Basi, wakamwoesha mwanamuke wake kwa kijana mumoja ambaye alikuwa rafiki ya Samusoni katika arusi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.