1Kisha kufa kwa Ahabu, watu wa Moabu waliasi wasitawaliwe na Israeli.
2Mufalme Ahazia alipokuwa Samaria alianguka kutoka chumba kilichokuwa juu ya paa ya nyumba yake, akaumia vibaya. Kwa hiyo akawatuma wajumbe, akawaambia: “Muende kwa Bali-Zebubu, mungu wa muji wa Ekuroni, mumwulize kama nitapona ugonjwa huu.”
3Lakini malaika wa Yawe akamwambia nabii Elia wa muji wa Tisibe, aende kukutana na wajumbe hao na kuwauliza: “Kwa nini munakwenda kwa Bali-Zebubu, mungu wa Ekuroni? Hakuna Mungu katika inchi ya Israeli?
4Mumwambie mufalme kwamba Yawe amesema hivi: ‘Hautashuka katika kitanda ulichopanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”
5Basi, Elia akawaendea. Wale wajumbe wakarudi kwa mufalme, naye akawauliza: “Mbona mumerudia?”
6Wakamujibu: “Tumekutana na mutu ambaye alitutuma turudi kukuambia kwamba Yawe amesema hivi: ‘Kwa nini unatuma wajumbe kwa Bali-Zebubu, mungu wa Ekuroni? Hakuna Mungu katika inchi ya Israeli? Hautashuka katika kitanda ulichopanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”
7Mufalme akauliza: “Ni mutu gani yule aliyekutana nanyi na kuwaambia mambo hayo?”
8Wao wakamujibu: “Alikuwa akivaa nguo ya manyoya na mukaba wa ngozi kwenye kiuno.”
Mufalme akasema: “Yule ni Elia wa Tisibe!”
9Halafu akamutuma kiongozi mumoja wa waaskari na watu wake makumi tano wamulete Elia.
Kiongozi huyo akaenda, akamukuta Elia akiikaa kwenye mulima, akamwambia: “Ewe mutu wa Mungu, mufalme anakuamuru ushuke.”
10Elia akamujibu yule kiongozi wa watu makumi tano: “Kama kweli mimi ni mutu wa Mungu, moto ushuke kutoka mbinguni na kukuteketeza wewe pamoja na watu wako!” Mara moja moto ukashuka kutoka mbinguni, ukamuteketeza pamoja na watu wake makumi tano.
11Mufalme akamutuma kiongozi mwingine na watu wake makumi tano wamulete Elia. Naye akamwambia Elia: “Ewe mutu wa Mungu, mufalme anakuamuru ushuke mara moja!”
12Elia akamujibu: “Kama kweli mimi ni mutu wa Mungu, moto ushuke kutoka mbinguni na kukuteketeza wewe pamoja na watu wako!” Mara moja moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamuteketeza pamoja na watu wake makumi tano.
13Kwa mara ingine tena, mufalme akatuma kiongozi mwingine na watu wake makumi tano. Kiongozi wa tatu akapanda kwenye mulima, akapiga magoti mbele ya Elia na kumusihi akisema: “Ewe mutu wa Mungu, ninakusihi uyahesabu maisha yangu na maisha ya hawa watumishi wako makumi tano yakuwe ya bei kali mbele yako.
14Viongozi wawili waliotangulia na watu wao, wameteketezwa na moto ulioshuka toka mbinguni; lakini sasa ninakuomba uhurumie maisha yangu.”
15Malaika wa Yawe akamwambia Elia: “Shuka pamoja naye, wala usimwogope.”
Basi, Elia akasimama, akashuka pamoja naye mpaka kwa mufalme.
16Akamwambia mufalme: “Yawe anasema hivi: ‘Kwa sababu ulituma wajumbe kuomba shauri kwa Bali-Zabubu mungu wa Ekuroni sawa vile hakuna Mungu katika Israeli ambaye ungemwomba shauri, basi, hautashuka katika kitanda ambacho umepanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”
17Kisha Ahazia akakufa kama vile Yawe alivyomwambia nabii wake Elia. Na kwa sababu Ahazia hakukuwa na mutoto mwanaume, Yoramu akakuwa mufalme kwa pahali pake, katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoramu mwana wa Yosafati, mufalme wa Yuda.
18Mambo mengine mufalme Ahazi aliyoyatenda yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.