Yoeli 4 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu atayahukumu mataifa

1Kwa wakati ule, na katika siku zile

nitakapowarudisha tena watu wa Yuda na Yerusalema

katika hali yao ya mbele,

2nitayakusanya mataifa yote,

niyapeleke katika bonde linaloitwa:

“Yawe anahukumu”.

Huko nitayahukumu mataifa hayo,

kwa mambo waliyowatendea watu wangu Waisraeli,

hao wanaokuwa mali yangu mimi mwenyewe.

Maana waliwatawanya kati ya mataifa,

waligawanya inchi yangu

3na kugawanya watu wangu kwa kupiga kura.

Waliuzisha vijana wanaume kwa kuhonga kahaba,

na wabinti kwa kupata divai.

4Munataka nini juu yangu enyi watu wa Tiro na Sidona na maeneo yote ya Filistia? Munataka kunilipiza kisasi? Kama munalipiza kisasi, mimi nitawalipiza mara moja!

11Mukuje upesi, enyi mataifa yote jirani,

mukusanyike kule katika bonde.

Ee Yawe!

Telemusha waaskari wako kuwashambulia!

12Mataifa haya yajiweke tayari;

yakuje kwenye bonde la Yawe Anahukumu.

Kule, mimi Yawe,

nitaikaa kwa kuyahukumu mataifa yote jirani.

13Mutwae kisu cha kuvuna,

maana sasa ni wakati wa mavuno.

Muingie! Muwapondeponde kama zabibu

ambazo zimejaza kikamulio.

Uovu wao umepita kipimo

kama mitungi inayofurika.

14Wanafika makundi kwa makundi

kwenye bonde la Hukumu,

maana siku ya Yawe imekaribia.

15Jua na mwezi vinatiwa giza,

na nyota zimeacha kuangaza.

Mungu atawabariki watu wake

16Yawe ananguruma kule Sayuni;

sauti yake inavuma kutoka Yerusalema;

mbingu na dunia vinatetemeka.

Lakini Yawe ni kimbilio la watu wake,

ni kikingio cha usalama kwa Waisraeli.

17Hapo, enyi Waisraeli,

mutajua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu,

ninakaa Sayuni, mulima wangu mutakatifu.

Muji Yerusalemu utakuwa muji mutakatifu;

na wageni hawatapita tena ndani yake.

18Wakati ule, divai mupya itatiririka juu ya milima,

na maziwa yatatiririka juu ya milima.

Vijito vyote vya Yuda vitajaa maji;

chemichemi itatokea ndani ya nyumba ya Yawe,

na kulinyweshea bonde la Sitimu.

19Misri itakuwa matongo,

Edomu itakuwa jangwa tupu,

kwa sababu waliwashambulia watu wa Yuda

wakawaua watu wasiokuwa na kosa.

20Lakini inchi ya Yuda itakaliwa na watu kwa milele,

na Yerusalema kwa kizazi hata kizazi.

21Nitawaazibu waliomwanga damu ya watu wa Yuda

wala sitawaachilia wenye makosa.

Yawe anakaa Sayuni.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help