1Mbele ya yote, ninawaonya ninyi kuwaombea watu wote. Muombe Mungu awasaidie na kuwabariki, na mumushukuru kwa ajili yao.
2Inafaa kuombea wafalme na watu wenye mamlaka kusudi tupate kuishi katika ukimya na amani katika kushikamana na ibada na katika mwenendo safi.
3Nalo jambo hilo ni zuri na lenye kupendeza Mungu Mwokozi wetu,
4anayetaka watu wote waokolewe na kuweza kutambua ukweli.
5Kwa maana kuna Mungu mumoja tu, na kuna mupatanishi mumoja tu kati ya Mungu na watu, ni yule mutu, Kristo Yesu,
6aliyejitoa mwenyewe kusudi awakomboe watu wote. Na huo ni ushuhuda kwa wakati uliopangwa, kwamba Mungu anataka kuwaokoa watu wake.
7Ni kwa hiyo nimewekwa kuwa mujumbe na mutume kwa kuwafundisha watu wa mataifa mengine kusudi wapate kumwamini Mungu na kutambua ukweli. Mimi ninasema ukweli wala si uongo.
8Basi, ninataka watu waombe Mungu wakiinua mikono juu, ikiwa imetakaswa, nao wafanye vile bila kasirani wala ubishi.
9Ninataka vilevile wanawake wavae kwa namna inayostahili. Inafaa wajipambe kwa adabu na kwa ukadirifu, si kwa namna mbalimbali za urembo za kusuka nywele, wala kwa zahabu, wala kwa ushanga au nguo za bei kali.
10Lakini kujipamba kwao kuwe matendo mema yanayostahili kutendwa na wanawake wanaojidai kwamba wanajitoa kwa kumwabudu Mungu.
11Wanawake wanapaswa kusikiliza mafundisho katika ukimya na utii kabisa.
12Lakini simupatii mwanamuke ruhusa ya kufundisha, wala ya kumutawala mwanaume, lakini akae katika ukimya.
13Kwa maana, Adamu ndiye aliyeumbwa wa kwanza, na kisha Eva.
14Na si Adamu aliyedanganywa, lakini ni mwanamuke ndiye aliyedanganywa na kuasi agizo la Mungu.
15Ingawa hivi mwanamuke ataokolewa kwa kuzaa watoto, kama akidumu katika imani, upendo na utakatifu na kuwa mukadirifu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.