Wagalatia 5 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Uhuru katika Kristo

1Kristo ametukomboa katika utumwa kusudi tukuwe huru kabisa. Basi, musimame imara wala musijitie tena katika vifungo vya utumwa.

2Musikilize! Mimi Paulo ninataka kuwaambia kwamba kama mukikubali kutahiriwa, Kristo hana mafaa yoyote kwenu.

3Mimi ninasema tena wazi, kila mutu anayekubali kutahiriwa sherti ashike Sheria yote.

4Kama munatafuta kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya kushika Sheria, mumejitenga mbali na Kristo na kujipotezea neema ya Mungu.

5Lakini sisi tunangojea kwa matumaini kwamba kwa uwezo wa Roho, tutahesabiwa haki kwa njia ya imani.

6Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.

7Ninyi mulikuwa na mwenendo muzuri! Ni nani aliyewazuiza kushika ukweli?

8Kishawishi hicho hakikutoka kwa Mungu anayewaita ninyi kuwa watu wake.

9“Chachu kidogo inachachisha donge zima.”

10Ingawa vile mimi niko na tumaini juu yenu kutoka kwa Bwana kwamba hamutakuwa na nia mbalimbali na mimi. Lakini yule anayewavuruga ataazibiwa hata ikiwa ni nani.

11Wandugu, ikiwa mimi ningali ninahubiri ya kama ni lazima kutahiriwa, basi kwa sababu gani ningali ninateswa? Kama ningefanya vile, basi watu hawangechukizwa na mahubiri yangu juu ya musalaba wa Kristo.

12Heri wale wanaoleta fujo kati yenu wangejikata viungo vyao vya uzazi.

13Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.

14Kwa maana Sheria yote inafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe.”

15Lakini kama mukiumana na kukulana kama nyama wa pori, muangalie vizuri musiteketezane.

Maisha ya kiroho na ya kimwili

16Mambo ninayotaka kusema ni haya: muishi chini ya uongozi wa Roho Mutakatifu, nanyi musitimize tamaa za kimwili.

17Kwa maana tamaa za kimwili zinapingana na tamaa za Roho Mutakatifu. Na tamaa za Roho zinapingana na tamaa za kimwili. Hao wawili wanapingana hata munashindwa kufanya sawa vile munavyotaka.

18Lakini kama mukiongozwa na Roho Mutakatifu, hamutaishi tena chini ya Sheria.

19Matendo ya kimwili yanajulikana wazi, nayo ndiyo uasherati, uchafu, kutawaliwa na tamaa za kimwili,

20kutambikia sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, kasirani, mapingano, matengano, ubaguzi,

21chuki, uuaji, ulevi, ulafi, na mambo mengine yanayofanana na hayo. Ninawaonya tena kama vile nilivyowaonya mbele, kwamba watu wanaotenda mambo kama hayo hawatashiriki katika Ufalme wa Mungu.

22Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,

23upole na kujizuiza. Hakuna Sheria inayokataza mambo kama hayo!

24Nao watu wa Kristo Yesu wameua hali yao ya kimutu pamoja na vifungo vyao vyote na tamaa zote mbaya.

25Kufuatana na vile tunavyoishi kwa nguvu za Roho, basi tufuate maongozi ya Roho vilevile.

26Tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help