Mezali 20 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Divai inaleta mazarau na kileo kinaleta ugomvi; yeyote anayevutwa navyo hana hekima.

2Kasirani kali ya mufalme ni kama simba anayenguruma; anayemukasirikisha anahatarisha maisha yake.

3Ni jambo la heshima kuepuka ugomvi; wapumbafu ndio wanaogombana.

4Muvivu halimi wakati wa kulima; wakati wa mavuno atatafuta lakini hatapata kitu.

5Mafikiri ya mutu ndani ya moyo wake ni kama kilindi cha maji; lakini mutu mwenye akili anajua kuyachota mule.

6Watu wengi wanajivunia kuwa wema, lakini mwaminifu wa kweli anapatikana wapi?

7Heri watoto wa mutu wa haki mwenye mwenendo mukamilifu!

8Mufalme anapoikaa kwa kutoa hukumu, anapepeta uovu wote kwa macho yake.

9Nani anayesubutu kusema: “Nimetakasa moyo wangu; mimi nimetakasika na zambi yangu?”

10Mizani danganyifu na vipimo danganyifu, vyote ni chukizo kwa Yawe.

11Hata mutoto anajulikana kwa matendo yake, kama ni safi na sawa.

12Sikio linalosikia na jicho linaloona, vyote viwili vimefanywa na Yawe.

13Usipende usingizi usikuje kuwa masikini; ukuwe macho nawe utakuwa na chakula kingi.

14Mununuzi analalamika: “Hakifai, hakifai,” lakini akiondoka anajisifu amepunguziwa bei.

15Kuna zahabu na wingi wa mawe ya bei kali; lakini kitu cha bei kali zaidi ni maneno ya maarifa!

16Mutu akiahidi kumukopesha mutu asiyejulikana, unyanganye nguo yake kuwa rehani.

17Chakula kinachopatikana kwa udanganyifu ni kitamu, lakini nyuma kinakuwa kama muchanga ndani ya kinywa.

18Mipango mizuri inafanyika kwa kushauriana; ukitaka kuanza vita inafaa kufikiri kwanza.

19Mupiga domo hafichi siri. Kwa hiyo umwepuke mutu wa kusemasema.

20Anayemulaani baba yake au mama yake, mwangaza wa uzima wake utazimika kama taa katika giza.

21Mali iliyopatikana kwa haraka kwa mwanzo, haitakuwa ya heri kwa mwisho.

22Usiseme: “Nitalipiza ubaya niliotendewa.” Umutegemee Yawe naye atakusaidia.

23Mizani danganyifu ni chukizo kwa Yawe, na vipimo visivyokuwa vya haki ni kitu kibaya.

24Hatua za mutu zinaongozwa na Yawe; mwanadamu anaweza namna gani kuelewa njia yake?

25Ni hatari kusema kwa muzaha “Nitamutolea Mungu hiki!” na kuanza kufikiri nyuma ya kufanya naziri ile.

26Mufalme mwenye hekima anapepeta waovu; anawaazibu bila huruma.

27Zamiri ya mutu ni taa ya Yawe; inachunguza nafsi ya mutu mpaka ndani kabisa.

28Wema na uaminifu unamukinga mufalme; utawala wake unaimarishwa kwa haki.

29Utukufu wa vijana ni nguvu zao. Uzuri wa wazee ni kichwa chenye imvi.

30Mapigo yanayoumiza ni dawa ya kuondoa uovu; fimbo inasafisha nafsi mpaka ndani kabisa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help