1Ole watoto waasi,
wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu,
wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu!
–Ni ujumbe wa Yawe.–
Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.
2Bila kutaka shauri langu, wanafunga safari kwenda Misri,
kukimbilia ulinzi kwa mufalme wa Misri,
kupata pahali pa kujificha katika inchi yake.
3Lakini ulinzi wa Mufalme wa Misri utakuwa haya yenu,
na kujificha katika inchi ya Misri kutakuwa fezeha yenu.
4Maana ingawa wakubwa wao wamefika Soani,
na wajumbe wao mpaka katika muji wa Hamesi,
5wote watapata haya. Wamisri hawawezi kuwasaidia ninyi,
hawawezi kuwapa musaada au faida,
lakini watawapatisha haya tu na kuwafezehesha.
6Ujumbe wa Mungu juu ya nyama wa pande za jangwa ya kusini:
Wajumbe wanapita katika inchi ya taabu na shida,
yenye simba, nyoka wa sumu na nyoka wakubwa wanaoruka.
Wamewabebesha punda na ngamia wao mali zao,
kuwapelekea watu wasioweza kuwafalia kitu.
7Maana musaada wa Misri ni bure, haufai kitu;
kwa hiyo nimeipanga Misri jina:
Nyoka mukubwa asiyekuwa na nguvu!
Watu wasiotii8Mungu aliniambia:
Sasa andika jambo hili mbele yao,
juu ya kibao na katika kitabu,
likuwe ushuhuda wa milele:
9Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminiwa;
watu wasiopenda kusikia mafundisho ya Yawe.
10Wanawaambia wale wanaopata maono hivi:
Musipate maono.
Wanawaambia manabii hivi:
Musitutangazie ukweli,
lakini mutuambie mambo ya kupendeza,
mutoe unabii wa mambo ya udanganyifu tu.
11Mugeuke na kuiacha njia ya ukweli;
musituambie tena juu ya Mungu, Mutakatifu wa Israeli.
12Kwa hiyo Mungu, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi:
Ninyi mumeukataa ujumbe wangu;
mukatumainia kutenda mabaya na kutengeneza udanganyifu.
13Basi, zambi hii itakuwa kwenu
kama ufa mukubwa katika ukuta murefu;
utabomoka mara moja na kuanguka chini kwa rafla.
14Kuporomoka kwa ukuta huo,
ni kama kupasuka kwa chungu
ambacho kimepasuliwa vibaya sana,
bila kubaki kigae cha kuopolea moto ndani ya jiko,
au kuchotea maji katika kisima.
15Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi:
Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa;
kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu.
Lakini ninyi hamukutaka.
16Pahali pake mulisema:
Hapana! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio.
Sawa, mutakimbia na farasi wenye mbio,
lakini farasi wa waadui zenu wana mbio zaidi.
17Watu wenu elfu moja watamukimbia askari mumoja adui;
na waaskari watano waadui watawakimbiza ninyi wote.
Kwa mwisho, watakaobaki,
watakuwa kama muti wa bendera kwa mulima,
kama kitambulisho kinachokuwa juu ya kilima.
Wakati wa wokovu18Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe,
atasimama na kuwaonea huruma.
Yawe ni Mungu wa haki.
Heri wote wale wanaomutumainia.
19Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.
Matengenezo makubwa20Ingawa Bwana atawakulisha chakula cha taabu na kuwakunywesha maji ya mateso, yeye ndiye Mwalimu wenu na hatajificha tena; nanyi mutamwona kwa macho yenu wenyewe.
21Mukienda kwa upande wa kuume au kushoto, mutasikia sauti nyuma yenu ikisema: Njia ni hii; muifuate.
22Mutazihesabu sanamu zenu za miungu zilizopakwa feza na zahabu kuwa uchafu. Mutazitupilia mbali kama takataka, mukisema: Mupotelee mbali!
23Mutakapopanda mbegu zenu, Yawe atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakomaa na kuwapa mavuno mengi mazuri. Makundi yenu ya nyama nao watakula katika mashamba makubwa ya kukulishia nyama.
24Ngombe dume na punda wenu wa kulima watapata malisho yaliyochaguliwa vizuri na kutiwa chumvi.
25Wakati utakapofika ambapo waadui watauawa na minara yao kubomolewa, vijito vya maji vitatiririka kutoka kila mulima na kilima.
26Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.
Mungu ataiazibu inchi ya Asuria27Muangalie, Yawe mwenyewe anakuja tokea mbali!
Amewaka hasira na moshi unafuka;
midomo yake inaonyesha kasirani yake,
maneno anayosema ni kama moto unaoteketeza.
28Pumzi yake ni kama mafuriko ya muto
ambao maji yake yanafika mpaka kwenye shingo.
Anakuja kupepeta mataifa kwa lungo ya maangamizi,
kuwafunga lijamu na kuwapeleka wasikotaka.
29Lakini ninyi watu wa Yerusalema mutaimba kwa furaha kama munavyofanya wakati wa makesha ya sikukuu. Mutajaa furaha kama watu wanaotembea kwa mudundo wa muziki wa filimbi kwenda kwenye mulima kwa Yawe, kikingio cha Israeli.
30Yawe atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa ndimi za moto mukali, ngurumo, zoruba na mvua ya mawe.
31Waasuria watajaa hofu watakaposikia sauti ya Yawe, wakati atakapowapiga na fimbo yake.
32Kila pigo la azabu ya Yawe juu ya Waasuria litaandamana na mudundo wa ngoma na zeze. Yeye mwenyewe atapigana na Waasuria.
33Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.