1Nyuma ya mambo hayo, Paulo akatoka Atene, na kwenda katika muji wa Korinto.
2Kule akakutana na Muyuda aliyeitwa Akila, muzaliwa wa jimbo la Ponto, na jina la muke wake lilikuwa Prisila. Katika siku zile walikuwa wangali wakitoka katika inchi ya Italia, kwa sababu mutawala Klaudio alikuwa ameamuru kwamba Wayuda wote watoke Roma. Paulo akaenda kuwatembelea kwao.
3Naye akakaa na kutumika pamoja nao, kwa maana wote walikuwa wafundi wa kutengeneza hema.
4Na kila siku ya Sabato, Paulo alibishana na Wayuda na Wagriki katika nyumba ya kuabudia na kuwashinda.
5Sila na Timoteo walipofika toka Makedonia, Paulo akajitolea sana kwa kuhubiri Neno la Mungu, akihakikisha kwa Wayuda kwamba Yesu ndiye Kristo.
6Lakini wakati Wayuda walipingana naye na kumutukana, kwa hiyo akakunguta mavumbi yaliyorukia juu ya nguo zake na kuwaambia: “Lazima ya kuazibiwa kwenu ikuwe juu ya kichwa chenu wenyewe! Mimi sina kosa. Tangu sasa nitawaendea watu wa mataifa mengine.”
7Halafu Paulo akaondoka pale, akaenda kukaa katika nyumba ya mutu mumoja aliyeitwa Tito Yusto, aliyekuwa mwenye kuogopa Mungu. Nyumba ya mutu huyu ilikuwa karibu sana na nyumba ya kuabudia.
8Na Krispo, mukubwa wa nyumba ya kuabudia, akamwamini Bwana pamoja na watu wote wa nyumba yake. Nao Wakorinto wengi waliomusikiliza Paulo wakaamini na kubatizwa.
9Siku moja usiku, Bwana akamwambia Paulo katika maono: “Usiogope, uendelee tu kusema, wala usinyamaze,
10kwa maana mimi ni pamoja nawe. Hakuna mutu katika muji huu atakayesubutu kukukamata kwa kukutendea vibaya, kwa maana ndani yake kutakuwa watu wengi watakaonigeukia.”
11Na Paulo akakaa kule kwa muda wa mwaka mumoja na miezi sita, akiwafundisha watu Neno la Mungu.
12Katika nyakati Galio alipokuwa liwali wa jimbo la Akaya, Wayuda wakamufanyia Paulo shauri baya kwa nia moja, wakamukamata na kumupeleka mbele ya tribinali,
13na kumushitaki: “Mutu huyu anawavuta watu kumwabudu Mungu kwa njia isiyopatana na Sheria yetu.”
14Paulo alipotaka kusema, Galio akawaambia Wayuda: “Kama mungemushitaki mutu huyu juu ya neno la uovu au kosa kubwa alilofanya, ningewasikiliza ninyi Wayuda vema.
15Lakini kwa kuona ni mabishano tu juu ya maneno, majina na sheria yenu, maneno yale yanawaangalia ninyi wenyewe. Mimi sitakata maneno yale.”
16Na kisha akawafukuza toka ndani ya tribinali.
17Basi wakamukamata Sositeni, mukubwa wa nyumba ya kuabudia, wakamupiga pale mbele ya tribinali. Lakini Galio hakushugulika na jambo hilo.
Paulo anarudi Antiokia18Paulo akaendelea kule Korinto kwa muda wa siku nyingi. Kisha akaagana na wandugu waamini, akasafiri kwa njia ya chombo na kwenda katika inchi ya Suria. Nao Prisila na Akila walikuwa pamoja naye. Mbele ya kuondoka, Paulo alinyolewa kwenye kivuko cha Kenkurea, kwa maana alikuwa ametimiza kiapo alichofanya mbele ya Mungu.
19Walipofika Efeso, Paulo akawaacha wale wenzake kule. Naye mwenyewe akaingia ndani ya nyumba ya kuabudia na kubishana na Wayuda.
20Nao wakamusihi akae nao muda murefu zaidi, lakini hakukubali.
21Alipoagana nao, akawaambia: “Kama Mungu akitaka nitarudi huku kwenu tena.”
Halafu akaondoka Efeso, akisafiri kwa njia ya chombo.
22Naye alipofika katika muji Kaisaria, akaenda Yerusalema kwa kusalimia kanisa. Kisha akaenda Antiokia.
23Alipokwisha kukaa Antiokia kwa siku chache, akaondoka kule, akapita muji kwa muji toka katika inchi ya Galatia mpaka katika inchi ya Furigia, na kule akawatia wanafunzi nguvu.
Apolo katika Efeso na Korinto24Katika siku zile, Muyuda mumoja, jina lake Apolo, muzaliwa wa muji Alesanduria, alikuwa amefika katika muji Efeso. Alikuwa mutu mwenye uwezo katika masemi na mwenye kuelewa sana Maandiko.
25Mutu huyu alikuwa amefundishwa Njia ya Bwana, naye alitangaza kwa bidii sana na kufundisha kwa ukweli habari za Yesu. Lakini alikuwa akijua tu ubatizo wa Yoane.
26Yeye akaanza kusema pasipo woga katika nyumba ya kuabudia. Prisila na Akila walipomusikia, wakaenda naye kwao na kumufasiria Njia ya Mungu kwa ukweli zaidi.
27Apolo alipotaka kwenda katika jimbo la Akaya, wandugu waamini wakamutia moyo, nao wakawaandikia wanafunzi wa kule kwamba wamukaribishe vizuri. Na wakati alipofika kule, akawasaidia sana wale walioamini kwa nguvu ya neema ya Mungu,
28kwa maana alibishana na Wayuda mbele ya watu wote na kuwashinda kabisa. Aliwaonyesha kwa njia ya Maandiko Matakatifu kwamba Yesu ndiye Kristo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.